-
Msemaji wa Serikali ya Iran: Marekani haina njia nyengine ghairi ya kurejea katika mapatano ya JCPOA
Mar 02, 2021 08:55Msemaji wa Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, siasa za mashinikizo ya kiwango cha juu zimefeli na Marekani haina njia nyingine ghairi ya kurejea katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Khatibzadeh: Huu si wakati mwafaka wa kuitishwa kikao cha JCPOA
Feb 28, 2021 23:44Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, kwa kutilia maanani misimamo na hatua za karibuni za nchi tatu za Ulaya na Marekani, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaona kuwa huu si wakati mwafaka wa kufanyika kikao kisicho rasmi kilichopendekezwa na Mkuu wa Siasa za Nje za Umoja wa Ulaya baina ya nchi hizo na Tehran kuhusu kadhia ya mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Iran: Njia nyepesi kwa Marekani kurejea katika JCPOA ni kuheshimu ahadi zake
Feb 28, 2021 09:48Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, njia sahali kabisa kwa Marekani kurejea katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ni kuheshimu na kufungamana na ahadi ilizotoa juu ya mapatano hayo ya kimataifa.
-
Ulaya na JCPOA; sharti la Iran la kurudi kwenye Protokali ya Ziada
Feb 25, 2021 13:34Jibu na radiamali ya pande za Ulaya na Marekani kwa hatua ya Iran ya kusimamisha utekelezaji wa hiari wa Protokali ya Ziada ya Mkataba unaopiga marufuku uundaji na uenezaji silaha za nyuklia y NPT ni ya kutafakariwa na inaonesha muelekeo na mtazamo usio wa kimantiki wa pande hizo.
-
Borrell akiri kuwa Iran inafungamana na mapatano ya JCPOA na kwamba Ulaya ndio inayoyakiuka
Feb 24, 2021 08:08Baada ya kujiondoa Marekani katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA, Umoja wa Ulaya na Troika ya Ulaya (Ujerumani, Ufaransa na Uingereza) zimekuwa na utendajikazi hasi katika uga wa kulinda mapatano hayo na pia katika kutekeleza ahadi zao. Hii ni Katika hali ambayo Iran imetekeleza ahadi zake kikamilifu katika mapatano ya JCPOA. Hivi sasa afisa wa ngazi za juu wa sera za kigeni katika Umoja wa Ulaya amekiri ukweli huo.
-
Iran: Muhula wa kusimamisha 'Protokali ya Ziada' unakaelekea kumalizika
Feb 21, 2021 04:24Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya kisiasa ameonya kuwa, iwapo Marekani haitachukua hatua yoyote ya kuliondolea vikwazo taifa hili kufikia kesho kutwa (Februar 23), basi Tehran itachukua hatua ya kusimamisha Protokali ya Ziada ya kupunguza kiwango cha uangalizi wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
UN yatoa mwito wa kuheshimiwa makubaliano ya JCPOA
Feb 20, 2021 09:13Naibu Msemaji wa Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amekaribisha hatua ya Marekani ya kumwandikia barua Rais wa Baraza la Usalama la umoja huo ya kuondoa madai ya serikali iliyotangulia ya nchi hiyo kuhusu kurejeshwa vikwazo vyote vya UN dhidi ya Iran.
-
Zarif: Marekani inapaswa kuondoa bila masharti yoyote vikwazo vyote vilivyowekwa na Trump
Feb 19, 2021 10:38Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Marekani inapaswa kuondoa bila masharti yoyote na kwa namna iliyo athirifu vikwazo vyote vilivyorejeshwa upya na kutekelezwa na aliyekuwa rais wa nchi hiyo Donald Trump.
-
Rouhani: Haiyumkiniki kujumuisha maudhui nyingine katika JCPOA
Feb 17, 2021 23:44Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema ni jambo lisilowezekana kuarifisha na kujumuisha maudhui nyinginezo katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Mashauriano ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani na Ufaransa kuhusu namna ya kulinda mapatano ya JCPOA
Feb 16, 2021 04:23Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani na Ufanrasa jana usiku walifanya mashauriano kuhusu masuala tofauti yakiwemo jinsi ya kulinda mapatano ya nyuklia ya JCPOA na vile vile hali ya msambao wa kasi wa virusi vya corona barani Ulaya.