-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu; fedheha ya kidemokrasia ya Marekani na mustakabali wa JCPOA
Jan 08, 2021 10:28Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa hotuba muhimu kwa mnasaba wa siku ya leo ya maadhimisho ya mapambano ya Dei 19 ya wananchi wa Qum dhidi ya utawala wa kiimla wa Shah ambapo ameashiria matukio ya hivi karibuni nchini Marekani, sharti la Iran la kurejea Washington katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na uwepo wa kieneo na uwezo wa kiulinzi wa Iran.
-
Iran yaanza kurutubisha urani kwa asilimia 20 katika kituo cha Fordow
Jan 04, 2021 12:16Msemaji wa serikali ya Iran ametangaza rasmi habari ya kuanza kurutubishwa tena madini ya urani kwa kiwango cha asilimia 20 katika kituo cha nyuklia cha Fordow, kilichoko kaskazini mashariki mwa mji wa Qum kusini mwa mji mkuu wa nchi hii, Tehran.
-
Ali Shamkhani: Chaguo pekee la Marekani ni kuondoa vikwazo vyote dhidi ya Iran
Jan 04, 2021 00:00Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kuwa, chaguo pekee la Marekani ni kuondoa vikwazo vyote dhidi ya Iran na hivyo kuachana na mkakati wake uliofeli wa mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Khatibzadeh: Mizozo ya Afghanistan inaweza kupatiwa ufumbuzi kwa njia za kisiasa
Dec 28, 2020 08:52Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, njia ya kuipatia ufumbuzi mizozo na mivutano inayoikabili Afghanistan ni utatuzi wa kisiasa.
-
Wabunge 150 wa Marekani wamtaka Biden airejeshe nchi hiyo katika JCPOA
Dec 24, 2020 04:44Wabunge 150 wa chama cha Democratic nchini Marekani wamemuandikia barua rais mteule wa nchi hiyo, Joe Biden wakiunga mkono azma yake ya kutaka kuirejeshe nchi hiyo kwenye makubaliano ya nyuklia ya JCPOA pasi na masharti yoyote mapya.
-
Marais wa Russia na Ufaransa wataka kulindwa mapatano ya JCPOA
Dec 23, 2020 08:55Marais Vladimir Putin wa Russia na Emmanuel Macron wa Ufaransa wametoa mwito wa kuweko jitihada za pamoja za kuyalinda mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
China: Chanzo cha matatizo ni Marekani kujitoa JCPOA na kuanzisha mashinikizo ya juu kabisa
Dec 22, 2020 09:19China imesisitiza kuwa, kurudi Marekani kwenye makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kuanza tena kutekeleza majukumu yake ndio njia sahihi na ya kimantiki ya kupunguza mivutano.
-
Zarif: Nchi za Ulaya zimekiuka wajibu wao katika JCPOA
Dec 22, 2020 00:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema data za miamala ya kibiashara baina ya nchi hii na Ulaya kati ya mwaka 2014 na 2019 zinaonesha wazi kuwa nchi tatu za Ulaya washiriki wa mapatano ya nyuklia ya JCPOA zilikiuka wajibu wao wa kisheria.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na kundi la 4+1 wasisitiza kulinda mapatano ya JCPOA
Dec 21, 2020 09:44Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na nchi zinazounda kundi la 4+1 wamesisitiza katika kikao chao juu ya kuyalinda mapatano ya JCPOA.
-
Guterres ataka nchi wanachama wa UN kushirikiana na Iran kibiashara
Dec 19, 2020 08:49Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza katika ripoti ya utekelezaji wa azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa juu ya udharua wa kulindwa mapatano ya JCPOA na kuzitaka nchi zote wanachama wa umoja huo kuanzisha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi na Iran kwa mujibu wa azimio hilo.