-
Iran: Kamwe hatutorudi nyuma katika kuyaunga mkono mataifa yanayodhulumiwa
May 28, 2018 21:09Mkuu wa Chombo cha Mahakama cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, Tehran kamwe haitolezegeza kamba katika kulinda malengo yake matukufu na thamani zake za kimsingi ikiwa ni pamoja na kuwaunga mkono wanyonge na kufanikisha malengo yake mengine ya Kiistratijia.
-
Umoja wa Ulaya: Tutayalinda mapatano ya nyuklia ya Iran licha ya Marekani kujitoa + Video
May 28, 2018 10:58Mkuu wa Sera za Kigeni za Umoja wa Ulaya amesema kuwa umoja huo umeazimia kikweli kweli kuyalinda mapatano ya nyuklia yaliyofikiwa mwaka 2015 baina ya Iran na kundi la 5+1, licha ya Marekani kujitoa katika mapatano hayo ya kimataifa.
-
Maendeleo yamepatikana katika mazungumzo ya nyuklia ya Iran na Ulaya
May 28, 2018 02:56Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema katika kipindi cha wiki mbili zilizopita kumepatikana maendeleo mazuri katika mazungumzo baina ya Iran na nchi za Ulaya kuhusu mapatano ya nyuklia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezwaji, JCPOA, lakini bado matoeko yanayofaa hayajapatikana.
-
Iran: Iwapo Ulaya inakusudia kupoteza wakati, basi Tehran haitoendelea na mazungumzo ya JCPOA
May 27, 2018 09:23Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Sayyed Abbas Araqchi amesema kuwa iwapo Tehran itahisi kwamba mazungumzo na Umoja wa Ulaya kuhusiana na kuendelea na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA yanaenda kinyume na makusudio au kwamba yanapoteza muda, basi haitoendelea na mazungumzo hayo.
-
Rais Rouhani: Hatua zilizochukuliwa hadi sasa ni chanya kwa ajili ya kuendeleza JCPOA
May 27, 2018 03:12Rais Hassan Rouhani amesema, baada ya Marekani kujitoa kwenye makubaliano ya JCPOA waliowengi katika jamii ya kimataifa wameipa haki Iran na kuyatetea makubaliano hayo na kuongeza kwamba hatua zilizochukuliwa hadi sasa ni nzuri kwa ajili ya kuendeleza makubaliano hayo ya nyuklia.
-
Zarif: Iran haijafanya mazungumzo na Ulaya kuhusu uwezo wake wa makombora na ushawishi kieneo
May 26, 2018 10:57Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekanusha kuwepo mazungumzo na nchi za Ulaya kuhusu uwezo wa makombora ya Tehran wala kuhusu ushawishi wake katika eneo.
-
Russia: Baada ya kujiondoa JCPOA, Marekani haina haki yoyote kuhusiana na makubaliano hayo
May 26, 2018 02:47Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imesisitiza kwamba kitendo cha Marekani kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya Iran maarufu kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA), kimeiondolea nchi hiyo haki yoyote kuhusiana na makubaliano hayo.
-
Sisitizo la Putin na Macron la kulindwa mapatano ya JCPOA
May 25, 2018 09:04Akizungumza mara tu baada ya kuonana na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, Rais Vladimir Putin wa Russia amesisitiza juu ya umuhimu wa kulindwa mapatano ya nyuklia kati ya Iran na nchi kubwa za dunia, mashuhuri kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) na kuusifu msimamo wa Ufaransa na nchi nyingine za Ulaya kuhusiana na kudumishwa utekelezaji wa mapatano hayo.
-
Mogherini: Kuyadumisha makubaliano ya JCPOA ni mtihani kwa Umoja wa Ulaya
May 24, 2018 22:49Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya amesema kuyalinda na kuyadumisha makubaliano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) ni mtihani kwa Umoja wa Ulaya.
-
Kiongozi Muadhamu: Ikiwa Ulaya itazembea, lran ina haki ya kuanzisha shughuli zake za nyuklia
May 24, 2018 00:21Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria uadui wa msingi, wa kina na endelevu wa Marekani dhidi ya mfumo wa Kiislamu na taifa la Iran na kusisitiza kwamba bila shaka Iran itaishinda tu Marekani iwapo viongozi wa Iran watatekeleza vilivyo majukumu yao.