Jul 25, 2020 02:43
Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala ya kimataifa amesema kuwa, kuuawa shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani ilikuwa jinai kubwa zaidi ya Marekani dhidi ya Iran baada ya Mapinduzi ya Kiislamu na kueleza kwamba, Iran italipa kisasi kwa mauaji hayo na hilo halina shaka.