-
Utambulisho halisi wa Marekani kwa mtazamo wa Kiongozi Muadhamu
Jun 21, 2018 02:40Kingozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei, Jumatano asubuhi alikutana na Spika wa Majlisi ya Kiislamu, Bunge la Iran, wabunge na wafanyakazi wa bunge ambapo alibainisha utambulisho na malengo halisi ya Marekani katika eneo.
-
Kiongozi Muadhamu: Sharti Wapalestina wenyewe waamue hatima ya Palestina
Jun 11, 2018 03:15Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema hatima ya Palestina inapaswa kuamuliwa na Wapalestina wenyewe, wakiwemo Waislamu, Wakristo na Mayahudi ambao wana asili na waliishi katika ardhi ya jadi ya Palestina.
-
Kiongozi Muadhamu: Ndoto ya maadui kuhusu JCPOA kamwe haitoaguliwa
Jun 04, 2018 12:13Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa ndoto waliyo nayo maadui kuhusu mapatano ya nyuklia ya JCPOA kamwe haitotimia. Amesema hayo leo katika kumbukumbu za mwaka wa 29 wa kufariki dunia Imam Khomeini MA, mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na huku akigusia mazungumzo ya nchi za Ulaya na Iran kuhusu mapatano ya hayo ya nyuklia amesema, taifa na serikali ya Iran haiwezi kukubaliana na vikwazo vya nyuklia na kwamba njozi ya maadui kuhusu JCPOA haitaaguliwa kwamwe.
-
Kiongozi Muadhamu: Ikiwa Ulaya itazembea, lran ina haki ya kuanzisha shughuli zake za nyuklia
May 24, 2018 00:21Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria uadui wa msingi, wa kina na endelevu wa Marekani dhidi ya mfumo wa Kiislamu na taifa la Iran na kusisitiza kwamba bila shaka Iran itaishinda tu Marekani iwapo viongozi wa Iran watatekeleza vilivyo majukumu yao.
-
Orodha mpya ya Makamanda Wapalestina ambao Israel inataka kuwaua; dalili ya uhai wa Israel kutegemea ugaidi
May 21, 2018 22:08Utawala wa Kizayuni wa Israel umetangaza orodha mpya ya makamanda wa Brigedi za Izzedin Qassam Tawi la Kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, ambao inalenga kuwaua kigaidi.
-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu: Ukombozi usioepukika wa Palestina, kushindwa kusikokwepeka kwa Marekani + Picha
May 18, 2018 13:54Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, Baytul Muqaddas ndio mji mkuu wa Palestina na kwa taufiki na uwezo wa Mwenyezi Mungu Palestina itakombolewa tu kutoka katika makucha ya maadui na kwamba Marekani na vitimbakwiri vyake hawawezi kufanya upuuzi wowote mbele ya uhakika na sunna hiyo ya Mwenyezi Mungu.
-
Kiongozi: Msiziamini nchi 3 za Ulaya katika mapatano ya JCPOA
May 09, 2018 09:34Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria baadhi ya matamshi kuhusu Iran kuendelea kuwepo katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA na nchi tatu za Ulaya na kusisitiza kuwa: "Kuhusu kufanya mazungumzo na nchi tatu za Ulaya, haipaswi kuziamiani na katika kila mapatano lazima kuwepo dhamana ya kweli na ya kivitendo la sivyo haiwezekani kuendelea kwa hali iliyopo."
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu la udharura wa kusimama kidete kukabiliana na njama za maadui
May 01, 2018 02:46Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kwa mnasaba wa maadhimisho ya Mei Mosi, Siku ya Wafanyakazi Ulimwenguni kwamba kuna udharura wa kusimama kidete kukabiliana na njama za maadui.
-
Kiongozi Muadhamu asisitiza juu ya mchakato endelevu na kuzidishwa uwezo wa jeshi la Iran
Apr 22, 2018 09:41Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Iran amepongeza na kusifu utendaji na uzoefu wa thamani wa wafanyakazi wa zamani wa jeshi na huku akieleza kuwa na matarajio kuhusu mustakbali mwema wa vijana jeshini amesisitiza kuwepo mchakato endelevu na kuzidishwa uwezo wa jeshi.
-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu kuhusu jinai ya Marekani, Uingereza na Ufaransa dhidi ya Syria
Apr 14, 2018 09:27Mapema leo Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameyataja mashambulizi yaliofanywa alfajiri ya leo na nchi za Marekani, Uingereza na Ufaransa dhidi ya Syria kuwa ni jinai na uhalifu na kusema kuwa: Marais wa Marekani na Ufaransa na Waziri Mkuu wa Uingereza ni wahalifu waliotenda jinai.