-
Kiongozi: Makundi ya kigaidi kama ISIS yametokana na uingiliaji wa madola makubwa
Nov 22, 2016 13:32Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria matukio machungu na ya kusikitisha katika eneo na nafasi ya baadhi ya madola makubwa katika kulazimisha ukosefu wa uthabiti na vita katika mataifa na kusistiza kuwa: "Jamhuri ya Kiislamu ya Iran daima imekuwa ikitoa wito kwa nchi zenye misimamo huru kuwa na nafasi yenye harakati katika kukabiliana na mashinikizo dhidi ya mataifa na inayataka yasikae kimya na kuwa watazamaji."
-
Ayatullah Khamenei: Iran haina hukumu yoyote kuhusu uchaguzi wa Marekani
Nov 16, 2016 10:55Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haina hukumu ya aina yoyote kuhusu uchaguzi wa rais wa Marekani na kuongeza kuwa, Iran daima imekuwa ikishuhudia uadui kutoka kwa vyama viwili vikuu vya Marekani.
-
Kiongozi Muadhamu: Muungano wa Magharibi hauna nia ya kweli ya kuutokomeza ugaidi
Oct 25, 2016 13:14Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema nchi zenye misimamo huru zinapaswa kuimarisha uhusiano baina yao na kutoathiriwa na siasa za madola ya Kiistikbari ili kuweza kuzima moto wa hitilafu na mapigano uliowashwa na madola hayo.
-
Kiongozi: Ni marufuku kwa Serikali, Bunge, Mahakama, vikosi vya ulinzi, kuingilia uchaguzi Iran
Oct 15, 2016 12:28Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametumia haki yake aliyopewa na kifungu nambari 110 cha Katiba, kuwasilisha siasa kuu za uchaguzi baada ya kushauriana na Halmashauri ya Kuainisha Maslahi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Kiongozi Muadhamu: Usalama ni moja ya nguzo kuu za ustawi na maendeleo ya Iran ya Kiislamu
Oct 04, 2016 11:37Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, amesema usalama ni moja ya nguzo kuu za ustawi na maendeleo ya Iran ya Kiislamu.
-
Kiongozi: Kuwakumbuka mashahidi ni nukta muhimu ya kukabiliana na njama za adui
Oct 02, 2016 10:26Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuhimiza kumbukumbu ya mashahidi ni moja ya nukta muhimu katika kukabiliana na njama za adui na kulinda mapambano katika jamii.
-
Kiongozi Muadhamu: Majeshi ya Iran yawe tayari kukabiliana na adui
Sep 28, 2016 10:26Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi yote ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuhusu ulazima wa majeshi nchini kujiimarisha kiitikadi, kielimu na kinidhamu sambamba na kuwapa wanajeshi vijana uzoefu wa zama za Kujihami Kutakatifu.
-
Hotuba ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi katika kubainisha tukio la Ghadir
Sep 21, 2016 04:40Kiongozi Maudhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, jana alikutana na maelfu ya wananchi wa matabaka mbalimbali kwa mnasaba wa Sikukuu ya Ghadir Khum ambapo mbali na kutoa mkono wa pongezi, heri na baraka kwa Waislamu alizungumzia umuhimu wa tukio la kihistoria la Ghadir katika pande tofauti.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu aupongeza msafara wa michezo ya Paralimpiki
Sep 19, 2016 09:33Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe kwa msafara wa michezo ya Paralimpiki wa "Mashahidi wa Mina" na kueleza kwamba:"Mliyofanya ni ya kujivunia na mumelifurahisha taifa la Iran".
-
Kiongozi Muadhamu: Kutoiamini hata chembe Marekani ni sehemu ya nguvu laini za Iran
Sep 18, 2016 10:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) ni "ngome imara ya Mapinduzi" na "chombo muhimu cha kulinda usalama wa ndani na nje".