-
Kifo cha kwanza cha mgonjwa na virusi vya Corona nje ya China charipotiwa Ufilipino
Feb 02, 2020 08:02Ufilipino imetangaza mapema leo Jumapili kwamba, imesajili kifo cha kwanza cha mtu aliyekuwa na virusi vya Corona nchini humo. Taarifa hiyo ya serikali ya Ufilipino imetolewa huku nchi mbalimbali duniani zikiwa katika pilikapilika na wasiwasi mkubwa kutokana na kasi ya kusambaa kirusi hicho hatari kinachoendelea kuua watu siku baada ya nyingine.
-
Kirusi cha Corona chafika Imarati, Taiwan na Sudan, idadi ya waliofariki dunia inaongezeka
Jan 29, 2020 10:45Kirusi hatari cha Corona kimeripotiwa kufika katika nchi za Imarati na Taiwan huku idadi ya watu wanaofariki dunia na kuambukizwa kirusi hicho ikiongezeka kwa kasi.
-
Nchi za Afrika zachukua tahadhari ya kukabiliana na virusi vya Corona
Jan 24, 2020 11:26Nchi za Afrika mashariki zimetangaza hatua na mipango ya kukabiliana na virusi vya Corona vinavyosababisha maradhi ya kupumua huku idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na mlipuko wa virusi hivyo nchini China ikiongezeka na kufikia 26.
-
"Kirusi cha China" chazusha hofu duniani, watu 6 wameaga dunia hadi sasa
Jan 21, 2020 09:11Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, litafanya kikao kesho Jumatano kutazama uwezekano wa kutangaza tahadhari ya kimataifa ya afya ya umma baada ya China kuthibitisha kwamba, kirusi hicho kinaambukizwa kupitia mawasiliano baina ya binadamu.
-
Angola yaripoti kesi mbili za kwanza za ugonjwa wa Zika
Jan 12, 2017 03:55Angola jana ilitangaza kuwa imesajili kesi mbili za awali za kirusi cha Zika, ikiwa imepita miezi mitatu baada ya kudhibitiwa mlipuko wa ugonjwa wa homa ya manjano ambao umeuwa nchini humo watu wasiopungua 400.
-
Kirusi cha Zika chahatarisha maisha ya watu bilioni 2 Afrika na Asia
Sep 03, 2016 02:35Uchunguzi umebaini kuwa, kirusi cha Zika kinahatarisha maisha ya watu zaidi ya bilioni mbili katika nchi kadhaa za mabara ya Afrika na Asia.
-
Kesi ya kwanza ya Zika yaripotiwa Guinea-Bissau
Jul 03, 2016 02:59Serikali ya Guinea-Bissau imebuni kamati ya dharura ya afya baada ya kuripotiwa kesi tatu za kwanza za kirusi hatari cha Zika.
-
Tahadhari ya WHO kuhusu Zika kwa waendao Olympiki Brazil
Jun 22, 2016 02:35Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa tahadhari ya afya kwa wote wanaokwenda kwenye mashindano ya Olimpiki nchini Brazili kufuatia mlipuko wa homa ya Zika.
-
Kirusi hatari cha Zika charipotiwa Afrika kwa mara ya kwanza
May 20, 2016 11:55Kirusi hatari cha Zika kimeripotiwa kuibuka barani Afrika kwa mara ya kwanza katika Visiwa vya Cape Verde magharibi mwa bara hilo.