Jul 08, 2017 03:46
Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki, IAEA, amesema Iran ambayo ni muathirika wa silaha za maangamizi ya umati, inaunga mkono kikamilifu mkataba mpya wa Umoja wa Mataifa kuhusu kupigwa marufuku silaha za nyuklia.