Apr 14, 2016 14:21 UTC
  • Upokonyaji silaha za nyuklia, takwa la kimataifa

Kupokonywa silaha za nyuklia Marekani na nchi nyingine zinazomiliki sialha hizo ni takwa na hitajio kuu la fikra za waliowengi ulimwenguni.

Gazeti la Resalat linalochapishwa mjini Tehran limeandika leo katika uchambuzi wake kuwa, kupokonywa silaha za nyuklia ni takwa ambalo nchi zinazomiliki silaha za aina hiyo, zikiongozwa na Marekani; zina hofu kubwa kuhusiana na mpango wa kutaka kutekelezwa hatua hiyo.

Gazeti la Resalat limeandika kuwa, kuwepo mamia ya vichwa vya nyuklia ni hatari kwa maisha ya mamilioni ya watu duniani na kwamba suala la kupokonya silaha za nyuklia linapasa kuwekwa katika ajenda ya kazi ya nchi mbalimbali duniani ili kudhamini usalama wa kimataifa.

Gazeti hilo linalochapishwa hapa Tehran limeendelea kuandika kuwa, nchi zinazomiliki silaha haribifu na zilizopigwa marufuku katika hatua yao inayokinzana waziwazi katika kikao cha hivi karibuni cha G-7 huko Hiroshima Japan, zimetaka kuwepo dunia pasina na silaha za nyuklia, katika hali ambayo nchi hizo hazistahiki kuzungumzia suala la kupokonywa silaha za nyuklia ulimwenguni.

Gazeti la Resalat limeongeza kuwa, hatua ya madola yanayomiliki silaha za nyuklia ya kutekelezwa miamala ya kindumakuwili kwa kupuuza maghala ya silaha za nyuklia yanayomilikiwa na utawala wa Kizayuni wa Israel, imeutia kiburi utawala huo na hivyo kutoheshimu taasisi yoyote ya kimataifa ukiwemo Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).

Tags