-
Telegraph: Vita dhidi ya Iran vinaweza vikawa moja ya makosa ya kihistoria
Aug 08, 2026 03:22Gazeti la Telegraph linalochapishwa nchini Uingereza limekiri katika ripoti yake kwamba Marekani na Israel zimeshindwa katika vita, huku Iran ikiwa imeibuka mshindi, na kwamba vita hivi vinaweza kuwa tukio muhimu sana la kupelekea kupungua satua na ushawishi wa Marekani duniani.
-
Trump anazidi kuchanganyikiwa kuhusu ulipizaji kisasi wa Iran, amkabili Hegseth kuhusu uhaba wa silaha
Aug 06, 2026 03:51Rais wa Marekani, Donald Trump, amezidi kukatishwa tamaa na kushindwa mara kwa mara kwa mashine ya kivita ya nchi hiyo kutokana na ulipizaji kisasi wa Iran na amemkabili Waziri wa Vita, Pete Hegseth, kuhusu uhaba wa silaha muhimu za Marekani.
-
Ripoti: Marekani inazishinikiza nchi za Afrika kujiondoa ICC au kukabiliwa na madhara
Aug 05, 2026 12:11Utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani unazishinikiza nchi za Afrika kujiondoa katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) na kutishia kuzichukulia hatua, huku Washington ikiongeza kasi ya kampeni yake dhidi ya mahakama hiyo.
-
Vyombo vya habari Ulaya vyafichua mpango wa kifisadi wa Rais wa FIFA na wandani wa Trump
Aug 05, 2026 02:38Jarida la The Times limefichua kiasi kikubwa cha fedha ambazo rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), Gianni Infantino, angeweka mfukoni iwapo mpango wa kuuza Kombe la Dunia ungetekelezwa.
-
Mshauri wa Kiongozi Muadhamu: Iran iliishinda Marekani katikati ya 'vita vya tatu vya Trump'
Aug 04, 2026 10:30Mohsen Rezaei, Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, amesema kuwa Marekani ilishindwa katikati ya "vita vya tatu vya Rais wa Marekani Donald Trump" dhidi ya Iran, huku vikosi vya ulinzi vya Iran vikivuruga mipango ya Marekani, kuilazimisha kuhamisha vituo vyake vya amri na wanajeshi wengi wa nchi hiyo wakiangamizwa na kujeruhiwa; hatua inayozidisha kushindwa kwingine kukubwa katika rekodi ya kufeli ya Marekani.
-
Muqawama wa Palestina watoa onyo baada ya mashambulizi mabaya zaidi ya Israel tangu kusitisha mapigano
Aug 03, 2026 10:10Makundi ya Muqawama ya Palestina yametoa onyo kali baada ya mashambulizi mabaya zaidi ya anga ya Israel tangu kusitisha mapigano Oktoba 2025, yakisema mashambulizi hayo yasiyokoma ni hujuma ya makusudi dhidi ya makubaliano ya kusitisha mapigano na ujumbe kwamba Israel haina nia ya kutimiza majukumu yake.
-
Sheikh Ibrahim Zakzaky apinga pendekezo la Trump kuhusu Gaza
Aug 03, 2026 02:46Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria, Sheikh Ibrahim Zakzaky, amelitaja pendekezo la Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu makubaliano ya usitishaji vita kati ya Israel na Hamas kuwa ni “uoga”, hasa kutokana na sharti linalodaiwa la kuitaka Hamas kusalimisha silaha zake.
-
Ripoti ya Middle East Monitor: Mwisho wa dhana ya Marekani ya 'kutoshindwa'
Aug 03, 2026 02:45Ripoti ya gazeti la Middle East Monitor imesema kuwa, Iran haiwezi kushindwa katika vita, na kwamba hali hiyo ni ukweli ambao Marekani na Israel haziwezi kuubadilisha hata kama watajitahidi kiasi gani.
-
New York Times: Umaskini wakithiri Marekani, pengo la kijamii lazidi kupanuka
Aug 03, 2026 02:43Gazeti la New York Times limeripoti kuongezeka umaskini nchini Marekani na kuongezeka pengo la kijamii miongoni mwa wananchi wa nchi hiyo.
-
Baada ya Iran kuapa kuwa itajibu mapigo makali, Trump asitisha mashambulizi dhidi ya miundombinu
Aug 02, 2026 13:15Rais wa Marekani Donald Trump amesema amefuta mashambulizi aliyotangaza kuwa yatafanywa dhidi ya Iran baada ya nchi za eneo kuomba yasitishwe wakati juhudi zinafanywa ili kufikia makubaliano, na kufuatia maonyo yaliyotolewa na Tehran kwamba uchokozi wowote mpya wa Marekani au Israel utakabiliwa na jibu la mapigo makali.