-
Kwa nini Trump ameshindwa kutatua migogoro ya kimataifa licha ya ahadi zote alizotoa?
Jun 05, 2025 05:58Katika makala yake iliyopitia miezi minne ya kwanza ya utawala wa pili wa Donald Trump, tovuti ya CNN imeandika kwamba kabla ya kuingia madarakani, rais huyo alijigamba kwamba alikuwa na uwezo wa kutatua matatizo na migogoro mikubwa ya dunia, lakini hali ya sasa sio nzuri hata kidogo, ingawa yeye si rais pekee wa Marekani kutoa ahadi za uongo kuhusu suala hilo.
-
Trump na matakwa ya kupindukia kwa Iran: Je, Washington inataka kufikia makubaliano au kutwisha matakwa?
Jun 05, 2025 04:15Rais Donald Trump wa Marekani amekariri matakwa ya kupindukia mipaka ya Washington kuhusu mpango wa amani wa nyuklia wa Iran kwa ajili ya kufikiwa mapatano ya pande mbili.
-
Afisa wa utawala wa Biden akiri Israel imefanya jinai Ghaza
Jun 03, 2025 07:03Msemaji wa zamani wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani amekiri hadharani kwa kusema: "Ni jambo lisilo na shaka kwamba Israel imefanya jinai ya kivita huko Gaza."
-
Je, kubadilika mkakati wa kijeshi wa Marekani barani Afrika, ni kurudi nyuma au kubadilishwa mbinu?
May 30, 2025 12:19Jeshi la Marekani linaendelea kubadilisha na kulegeza misimamo yake ya awali kuhusu "utawala bora" barani Afrika na kukabiliana na vyanzo vya uasi na machafuko, na sasa linasisitiza kwamba serikali dhaifu za Kiafrika zinazoshirikiana na Marekani zinapasa kujitegemea zenyewe kijeshi na kiusalama.
-
Je, utawala wa Trump unataka kubadilisha kisiasa mazingira ya vyuo vikuu vya Marekani?
May 30, 2025 03:05Kutokana na hali ya mvutano inayoendelea kati ya utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani na Chuo Kikuu cha Harvard, serikali imetaka kufutwa kwa kandarasi zote za kifedha na chuo hicho.
-
Onyo la Trump kwa Netanyahu baada ya kutishia kuishambulia Iran
May 29, 2025 06:17Rais wa Marekani, Donald Trump ameripotiwa kuvutana na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu katika mazungumzo yao ya simu, baada ya nduli huyo wa vita wa utawala wa Kizayuni kutishia kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran, na hivyo kuhatarisha mazungumzo ya kidiplomasia yanayoendelea kati ya Tehran na Washington.
-
Hamas yaafiki pendekezo la US la kuondoka askari wote wa Israel Gaza
May 29, 2025 06:07Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema imefikia makubaliano na Mjumbe Maalum wa Marekani katika eneo la Asia Magharibi, Steve Witkoff kuhusu "mfumo jumla" wa kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza.
-
Russia yajibu baada ya Trump 'kumtishia nyau' Putin eti 'anacheza na moto'
May 28, 2025 06:48Rais wa Marekani, Donald Trump ametoa matamshi ambayo yanaonekana ya kumtishia mwenzake wa Russia, Vladimir Putin, ambapo amesema "anacheza na moto," bila kufafanua nini hasa anamaanisha.
-
Je, kwa nini uadilifu wa rangi ni nara tupu isiyotekelezeka huko Marekani?
May 28, 2025 06:02Miaka mitano baada ya kuuawa kikatili George Floyd, kijana Mmarekani mweusi, na polisi wa nchi hiyo, hatua na sera zilizoahidiwa kutekelezwa na serikali ya Marekani na makampuni mengi makubwa ya kiuchumi nchini humo kwa ajili ya hakikisha haki na usawa vinadumishwa kati ya jamii na watu wa rangi tofauti wa nchi hiyo zimesahaulika kabisa.
-
Kwa nini Trump ana vigezo vya kibaguzi kuhusu suala la nyuklia?
May 26, 2025 02:14Siku ya Ijumaa, Mei 23, Rais Donald Trump wa Marekani alitia saini dikri mpya kadhaa zinazolenga kuongeza uwezo wa uzalishaji wa nishati ya nyuklia, kupunguza kanuni za udhibiti na kupanua sekta ya urutubishaji wa madini ya urani nchini humo.