-
Walibya: Serikali ya Dbeibah itimuliwe kwa kuvuka mistari myekundu
Aug 29, 2023 08:19Viongozi na wanasiasa mashuhuri wa Libya wametoa mwito wa kuondolewa mamlakani serikali nzima ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Abdul Hamid Dbeibah, baada ya kufichuka habari ya Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo kuonana kwa siri na waziri wa mambo ya nje wa utawala wa Kizayuni, Eli Cohen nchini Italia.
-
Muqawama wa Palestina wawapongeza wananchi wa Libya
Aug 28, 2023 23:15Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa shukrani rasmi kwa wananchi wa LIbya kwa hatua yao ya kuonesha msimamo imara wa kulaani hatua ya waziri wa mambo ya nje wa Libya ya kuonana na waziri wa mambo ya nje wa Israel.
-
Waziri wa Libya akimbia nchi baada ya kusimamishwa kazi, hasira zinaendelea
Aug 28, 2023 08:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Libya, Najla al Mangoush amekimbilia Uturuki baada ya Mkuu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya kumsimamisha kazi kwa kosa la kuonana na waziri wa mambo ya nje wa utawala wa Kizayuni nchini Italia.
-
Italia yazilaumu nchi za Magharibi kwa kuivamia kijeshi Libya wakati wa Gaddafi
Aug 18, 2023 01:06Waziri wa Mambo ya Nje ambaye pia ni Naibu Waziri Mkuu wa Italia amezilaumu nchi za Magharibi kwa kuivamia kijeshi Libya wakati wa harakati za wananchi za kuipindua serikali ya kiongozi wa muda mrefu Muammar Gaddafi lakini ameshindwa kulaumu uharibifu mkubwa uliofanywa na madola hayo ya Magharibi katika uvamizi wao huo.
-
Waliouawa katika mapigano ya pande hasimu za jeshi Libya wafika 55
Aug 16, 2023 23:46Idadi ya waliouawa katika mapigano baina ya pande mbili hasimu za kijeshi katika mji mkuu Libya, Tripoli imeongezeka na kufikia watu 55.
-
Mapigano ya utumiaji silaha yaanza tena katika mji mkuu wa Libya, Tripoli
Aug 15, 2023 23:19Msemaji wa masuala ya dharura na utoaji misaada nchini Libya ametangaza kuwa mapigano ya utumiaji silaha yameanza tena katika mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli.
-
Libya, familia za wahanga waliozikwa kwenye makaburi ya umati zataka wahusika wanyongwe
Aug 14, 2023 08:51Familia za watu waliouawa na kuzikwa kwenye makaburi ya halaiki zimepinga adhabu ya vifungo vya jela kwa wale waliohusika na mauaji ya mamia ya raia na kuzikwa kwenye makaburi hayi katika mji wa Tarhuna, kusini mashariki mwa mji mkuu wa Libya, Tripoli, na badala yake zinataka wapewe adhabu ya kifo
-
Maiti 27 za wahajiri zapatikana jangwani karibu na mpaka wa Tunisia
Aug 10, 2023 22:49Mamlaka za Libya zimetangaza habari ya kugunduliwa miili 27 ya wahajiri wa Kiafrika katika jangwa la magharibi karibu na mpaka wa nchi hiyo na Tunisia.
-
Iran na Libya zatangaza azma ya kuimarisha uhusiano
Jul 25, 2023 11:49Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran na Libya wamesisitiza azma ya viongozi wa nchi mbili ya kupanua uhusiano wa pande mbili.
-
Libya yawahukumu watu 37 kwa kusababisha vifo vya wahamiaji 11
Jul 11, 2023 07:32Mahakama nchini Libya imeidhinisha hukumu kali kwa watu 37 waliotuhumiwa kujihusisha na magendo ya binadamu. Watu hao wanatajwa kusababisha vifo vya wahajiri waliokuwa wakijaribu kuelekea Ulaya kupitia Bahari ya Mediterania. Haya yameelezwa na Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Libya.