-
'Kimbunga cha Bomu' chaua watu 28 Marekani, nyumba milioni 1.8 zakosa umeme
Dec 25, 2022 09:50Makumi ya watu wamepoteza maisha huku mamilioni ya wengine wakiathiriwa moja kwa moja na kimbunga kikali kilichokumba majimbo kadhaa ya Marekani wakati huu wa msimu wa baridi kali.
-
Marekani yakataa kujibu barua ya maripota wa UN kuhusu vikwazo dhidi ya Iran
Dec 25, 2022 08:28Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekuwa chini ya vikwazo vya upande mmoja vya Marekani kwa zaidi ya miaka 40. Kuwekwa vikwazo dhidi ya Iran katika kipindi cha uongozi wa Donald Trump, rais wa zamani wa Marekani baada ya kujitoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kuanzisha kampeni ya mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa, kumezidisha vikwazo visivyo na kifani vya nchi hiyo dhidi ya taifa la Iran.
-
Iran: Rais wa Ukraine ajifunze kwa hatima ya viongozi walioitegemea US
Dec 22, 2022 23:43Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amepuuzilia mbali madai yasiyokuwa na msingi kwamba Tehran imeipa Moscow ndege zisizo na rubani kwa ajili ya kuzitumia katika vita dhidi ya Ukraine na kusisitiza kuwa, Rais wa Volodymyr Zelensky wa Ukraine anapaswa kupata somo kutokana na hatima iliyowafika viongozi mbalimbali waliotegemea misaada ya Marekani.
-
Twitter yashirikiana na Wizara ya Ulinzi ya Marekani kuanzisha akaunti feki duniani kote
Dec 22, 2022 06:18Ufichuzi mpya unaonyesha kuwa licha ya madai ya mtandao wa kijamii wa Twitter kufuta mitandao ya siri ya matangazo ya serikali ya Marekani, mtandao huo unashirikiana na Wizara ya Ulinzi ya Marekani kuzindua akaunti za watumiaji bandia duniani kote.
-
Marekani yaiwekea vikwazo vipya Iran, vyajumuisha Mwendesha Mashtaka Mkuu
Dec 22, 2022 04:09Wizara ya Fedha ya Marekani imeiwekea Iran vikwazo vipya kwa kisingizio cha ukiukaji wa haki za binadamu, katika kuendeleza uingiliaji wake wa masuala ya ndani ya Iran na kutekeleza sera ya mashinikizo ya juu zaidi dhidi ya Tehran.
-
Matukio ya Ukraine na sisitizo la Macron la kupewa dhamana ya usalama Russia
Dec 22, 2022 03:47Vita vya Ukraine vinaendelea kama vilivyo licha ya kuingia mwishoni mwa mwezi wake wa 10 tangu vianze, na hakuna ishara zozote za kumalizika karibuni vita hivyo. Kinachoonekana kwenye matukio ya hivi sasa ni kuzidi kuwa vikali tu vita hivyo.
-
Russia: Jinai za kivita za Marekani na Nato Afghanistan zimepuuzwa
Dec 21, 2022 03:54Mwakilishi wa Kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa amesema katika kikao cha Baraza la Usalama la umoja huo kuwa jinai za kivita za Marekani na Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (Nato) huko Afghanistan zimepuuzwa.
-
Jenerali Qaani: Wamarekani si watu wa uwanja wa vita
Dec 21, 2022 00:51Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema kuwa mapambano au muqawama ni miongoni mwa kanuni zinazosisitizwa katika dini ya Kiislamu na kusema: "Wamarekani si watu wa medani ya vita na wameshindwa katika medani kuu."
-
Iran: Marekani ikhitari diplomasia badala ya mashinikizo na vitisho
Dec 20, 2022 04:18Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema iwapo Marekani inataka kweli kuhuisha makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, haina chaguo jingine isipokuwa kukhitari njia ya diplomasia badala ya mashinikizo, vitisho na makabiliano.
-
Russia yatungua makombora ya Marekani ya HARM
Dec 20, 2022 03:53Russia imesema vikosi vyake vya ulinzi wa anga vimefanikiwa kutungua makombora manne yaliyotengenezwa na Marekani ya HARM, katika anga ya eneo la Belgorod.