-
Hizbullah: Marekani, Saudia wahusika wakuu wa vita vya kiuchumi dhidi ya Lebanon
Jan 15, 2022 23:14Naibu Mkuu wa Baraza la Utendaji la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbuullah ya Lebanon amesisitiza kuwa, Marekani na Saudi Arabia zimeanzisha vita vya kiuchumi dhidi ya Lebanon.
-
Kukosolewa vikali rekodi ya haki za binadamu ya serikali ya Biden
Jan 15, 2022 23:13Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limekosoa rekodi ya haki za binadamu ya serikali ya Rais Joe Biden wa Marekani na kuitaja kuwa inatia wasiwasi. Human Rights Watch imebainisha hayo katika ripoti yake ya hali ya haki za binadamu duniani katika kipindi hiki cha mwanzoni mwa mwaka mpya wa 2021.
-
Kambi ya jeshi la US nchini Iraq yashambuliwa kwa droni
Jan 15, 2022 08:43Uwanja wa ndege za kijeshi wa Marekani wa Balad ulioko kaskazini mwa mji mkuu wa Iraq, Baghdad umeshambuliwa kwa ndege zisizo na rubani.
-
Taliban yaitaka US iheshimu wito wa UN wa kuachia fedha za Afghanistan
Jan 14, 2022 21:16Serikali ya Taliban imeitaka Washington itekeleze mwito uliotolewa hivi karibuni na Umoja wa Mataifa, wa kuachia fedha za Afghanistan zilizozuiwa nchini Marekani.
-
Iran: Marekani haina azma ya kufunga jela ya Guantanamo
Jan 13, 2022 23:23Mkuu wa Masuala ya Kimataifa wa Idara ya Mahakama ya Iran ameukosoa vikali utawala wa Rais Joe Biden wa Marekani kwa kufeli kutekeleza ahadi yake ya kufunga jela ya kutisha ya Guantanamo Bay iliyoko nchini Cuba.
-
Brigedia Jenerali Shekarchi: Marekani ni mfadhili mkuu wa ugaidi, chanzo cha ukosefu wa usalama duniani kote
Jan 11, 2022 10:46Msemaji wa Jeshi la Iran ameitaja Marekani kuwa nchi inayoongoza kwa kufadhili ugaidi duniani na kusema Washington ndiyo chanzo cha ukosefu wa usalama kote duniani.
-
Uchunguzi: Wabunge 1,700 wa Kongresi ya US wamewahi kumiliki watumwa
Jan 11, 2022 04:22Uchunguzi mpya umefichua kuwa, zaidi ya watu 1,700 waliowahi kuhudumu katika Kongresi ya Marekani wamewahi kuwamiliki wanadamu kama bidhaa, hali inayoonesha biashara ya utumwa ilivyokuwa imekita mizizi nchini humo.
-
Waliohukumiwa kifo Marekani wafadhilisha 'risasi' badala ya sindano ya sumu
Jan 11, 2022 04:20Wafungwa wawili waliohukumiwa kifo katika jimbo la Oklahoma nchini Marekani wameenda mahakamani kutaka kuangaliwa upya namna ya utekelezaji wa hukumu ya kifo nchini humo.
-
Wataalamu wa UN waitaka Marekani ifunge gereza la Guantamano
Jan 11, 2022 04:19Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wameutaka utawala wa Rais Joe Biden wa Marekani utekeleze ahadi yake ya kufunga jela ya kutisha ya Guantanamo Bay iliyoko nchini Cuba.
-
Wanajeshi magaidi wa Marekani waiba makumi ya malori ya mafuta ya Syria
Jan 10, 2022 08:33Duru za kiusalama za Syria zimetangaza kuwa, muungano vamizi unaoongozwa na wanajeshi magaidi wa Marekani umeiba malori mengine 79 ya mafuta ya Syria na kuyaingiza nchini Iraq.