-
Watu 35 wameuawa katika matukio ya ufyatuaji risasi nchini Marekani
Aug 14, 2017 10:47Kituo cha takwimu za matukio ya ukatili wa utumiaji silaha moto nchini Marekani kimetangaza kuwa watu 35 wameuliwa kwenye matukio ya ufyatuaji risasi katika maeneo tofauti nchini humo.
-
Korea Kaskazini: Njia pekee ya kuzuia vita katika eneo ni Seoul kuzuia chokochoko za Marekani
Aug 13, 2017 23:11Serikali ya Korea Kaskazini imekosoa mazungumzo ya simu ya Rais Moon Jae-in wa Korea Kusini na Rais Donald Trump wa Marekani yaliyofanyika hivi karibuni na kusema kuwa mazungumzo hayo hayawezi kusaidia kumaliza mgogoro uliopo.
-
Meja Jenerali Jaafari: Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni chimbuko la heshima izza ulimwenguni
Aug 13, 2017 23:05Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, SEPAH, amesema kuwa, kuwa mfuasi wa Mapinduzi ya Kiislamu ni fakhari kwa watu huru duniani na kwamba, mapinduzi haya ni chimbuko la izza na heshima ulimwenguni.
-
Lavrov: Muelekeo wa Marekani wa kupambana na ugaidi ni wa kindumakuwili
Aug 13, 2017 03:40Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergei Lavrov, amesema muelekeo na mtazamo wa Marekani kuhusiana na ugaidi ni wa kindumakuwili na kubainisha kuwa muungano unaoitwa wa kimataifa wa kupambana na Daesh (ISIS) chini ya uongozi wa Marekani sio tu haupambani na kundi la kigaidi la Jabhatu-Nusrah bali unafanya jitihada pia za kulilinda kundi hilo.
-
Mamilioni ya wapiganaji wa kujitolea Korea Kaskazini wajiweka tayari kupambana na Marekani
Aug 12, 2017 23:18Vyombo vya habari nchini Korea Kaskazini vimeripoti kwamba karibu watu milioni 3.5 wa kujitolea wametangaza utayarifu wao kwa ajili ya kupambana na Marekani vitani.
-
Indhari ya Ujerumani na Russia kuhusu hatari ya kutokea vita kati ya Marekani na Korea Kaskazini
Aug 12, 2017 09:02Kuongezeka mivutano na kutoleana kauli za vitisho viongozi wa Marekani na Korea Kaskazini kumeitia wasiwasi mkubwa jamii ya kimataifa juu ya uwezekano wa kutokea vita katika eneo la Mashariki mwa Asia.
-
Marekani yaua raia 16 katika hujuma ya anga Afghanistan
Aug 12, 2017 02:29Kwa akali raia 16 wameuawa kufuatia shambulizi la anga la muungano wa kijeshi wa nchi za Magharibi unaoongozwa na Marekani nchini Afghanistan.
-
Majibu ya Iran kwa Kongresi ya Marekani, Washington inavuruga usalama M. ya Kati
Aug 11, 2017 21:48Kamati ya Usalama wa Taifa na Siasa za Nje ya Bunge la Iran imepasisha mpango kamili wa kukabiliana na chokochoko na ugaidi wa Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Nchi za Ulaya zaendelea kupinga vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Russia
Aug 10, 2017 23:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Sigmar Gabriel amesema kuhusu vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Russia kwamba, hatua mpya za Marekani za kutaka kuibana zaidi Russia zinaweza kusababisha matatizo katika umoja wa nchi za Magharibi kuhusu mgogoro wa Ukraine.
-
Iran: US ijiandae kwa matokeo mabaya ikikiuka JCPOA
Aug 09, 2017 03:08Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameitahadharisha Marekani na matokeo mabaya itakayoyapata iwapo itaamua kukiuka makubaliano ya nyuklia ya Vienna.