-
Hofu ya Amnesty International baada ya Misri kupewa uenyekiti wa AU
Feb 09, 2019 04:26Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeeleza wasi wasi wake baada ya Misri kuteuliwa kuwa mwenyekiti wa kiduru wa Umoja wa Afrika kwa mwaka huu 2019, likisisitiza kuwa ukandamizaji wa haki za binadamu umefikia katika upeo wa juu kabisa katika kipindi cha utawala wa Rais wa sasa wa nchi hiyo, Abdul Fattah al Sisi.
-
Nchi tatu za Afrika zataka Russia iwepo kijeshi katika ardhi zao
Feb 05, 2019 23:16Libya, Sudan na Misri, nchi tatu za Kiarabu za bara la Afrika zimetangaza utayari wa kuwapokea askari wa Russia au kuiruhusu nchi hiyo ianzishe kituo cha kijeshi katika ardhi zao.
-
Bunge la Misri lajadili hoja ya kuondoa kikomo cha muhula wa rais
Feb 05, 2019 12:19Bunge la Misri leo Jumanne limeanza kujadili hoja ya kuondoa kikomo cha muhula wa rais, hatua ambayo huenda ikamruhusu Rais Abdulfattah al-Sisi wa nchi hiyo agombee zaidi ya mihula miwili iliyoruhusiwa na katiba.
-
Libya yaanza ujenzi wa ukuta katika mpaka wa pamoja na Misri
Jan 22, 2019 11:29Serikali ya Libya imeanzisha ujenzi wa ukuta katika mpaka wa pamoja na Misri kwa lengo la kuzuia kuingia wanachama wa kigaidi katika nchi hiyo.
-
Magaidi sita waangamizwa na maafisa usalama kusini mwa Misri
Jan 13, 2019 04:20Wanachama sita wa genge moja la kigaidi wameuawa katika operesheni ya maafisa usalama huko kusini mwa Misri.
-
Misri kuanzisha kivuko cha kibiashara kati yake na Ghaza
Jan 12, 2019 23:29Mwakilishi wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) ametangaza habari ya kuanzishwa kivuko cha kibiashara katika mpaka wa Ukanda wa Ghaza na Misri.
-
Amnesty: Ukandamizaji umefikia kileleni Misri katika utawala wa al Sisi
Jan 05, 2019 11:49Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeripoti kuwa, ukandamizaji wa haki ya kujieleza umefikia kileleni katika kipindi cha utawala wa Rais wa sasa wa Misri, Abbel Fattah al Sisi.
-
CBS: Misri na Israel zina ushirikiano wa karibu wa kijeshi
Jan 05, 2019 04:27Rais Abdel Fattah el-Sisi wa Misri ameiomba kanali ya televisheni ya CBS ya Marekani kutorusha hewani mahojiano iliyomfanyia, ambapo alifichua kuhusu uhusiano wa karibu wa kijeshi wa nchi hiyo na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Iran yalaani shambulizi la kigaidi dhidi ya watalii nchini Misri
Dec 30, 2018 11:07Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani shambulizi la kigaidi la hivi karibuni lililopelekea kuuawa watalii kadhaa huko nchini Misri.
-
Watu kadhaa wakiwemo watalii wauawa katika mripuko wa bomu Misri
Dec 29, 2018 04:32Watalii watatu wa Vietnam na raia mmoja wa Misri wameuawa baada ya bomu lililotegwa kando ya barabara kuripukia basi lililokuwa likifanya safari ya kitalii karibu na Mapiramidi ya Giza nje kidogo ya mji mkuu wa Misri, Cairo.