-
Rais Pezeshkian: Uhusiano mzuri baina ya nchi za Kiislamu utazima njama za maadui
Dec 19, 2024 00:13Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema "kadiri tutavyoweza kuboresha uhusiano wetu na nchi za Kiislamu ndivyo tutakavyoweza zaidi kuzima njama za maadui dhidi yetu".
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran aelekea Misri kushiriki kikao cha D-8
Dec 17, 2024 23:35Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameelekea mjini Cairo Misri kwa ajili ya kushiriki kwenye kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa kundi la D-8 la nchi za Kiislamu zinazostawi.
-
Mgombea urais wa chama kikuu cha upinzani Namibia: Hatutayakubali matokeo ya uchaguzi
Dec 01, 2024 02:43Mgombea mkuu wa urais wa upinzani nchini Namibia, Panduleni Itula, amesema chama chake hakitatambua matokeo ya uchaguzi uliokumbwa na utata wa kuongezewa muda wa upigaji kura na kutawaliwa na fujo na madai ya uchakachuaji.
-
Mbunge wa UK: FIFA na UEFA zina 'nyuso mbili za ubaguzi wa rangi' kwa maslahi ya Israel
Nov 14, 2024 02:38Mbunge wa chama cha Leba nchini Uingereza Zarah Sultana amekosoa vikali mashirikisho ya juu ya soka duniani ya FIFA na UEFA kwa kutoziadhibu timu za soka za Israel wakati utawala huo wa Kizayuni unaendeleza mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.
-
UN: Nchi zinazohusika ziache kuzipatia silaha pande zinazopigana nchini Sudan
Nov 13, 2024 08:26Umoja wa Mataifa umesema, kuendelea kuwasambazia silaha askari wa jeshi na wa vikosi vya wanamgambo wanaopigana nchini Sudan ndiko "kunakowezesha kufanyika uchinjaji" na lazima kukomeshwe wakati raia wa nchi hiyo wanaendelea kubeba mzigo mkubwa wa vita.
-
Iran yaendelea na jitihada za kusimamishwa vita Ghaza na Lebanon
Oct 31, 2024 03:41Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo na mawaziri wenzake wa mambo ya nje wa Misri, Indonesia na Qatar na kujadiliana nao masuala ya kikanda na uhusiano wa pande mbili ikiwa ni muondelezo wa jitihada za Iran za kuhakikisha vita vinakomeshwa huko Ghaza na Lebanon.
-
Iran na Misri zataka Israel ilazimishwe kukomesha jinai zake Gaza, Lebanon
Oct 24, 2024 02:48Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian na mwenzake wa Misri, Abdel Fattah El-Sisi wamesisitiza kuwa uchokozi wa Israel katika Ukanda wa Gaza na Lebanon ni lazima usitishwe, na kutoa wito wa kuwepo juhudi za kuzuia kuenea kwa mzozo katika maeneo mengine ya eneo la Asia Magharibi.
-
Iran na Misri zajadili masuala ya kikanda na kimataifa
Oct 17, 2024 23:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Misri Abdel Fattah el-Sisi; ambapo wamejadili masuala muhimu ya kikanda na uhusiano wa pande mbili.
-
Marekani kuiuzia Misri makombora ya dola milioni 740
Sep 26, 2024 00:29Serikali ya Marekani imeidhinisha mauzo ya makombora yenye thamani ya mamilioni ya dola kwa Misri licha ya serikali ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika kuendelea kuandamwa na shutuma za ukiukaji wa haki za binadamu.
-
Iran: Tuna haki ya kujibu mapigo ya mauaji ya kigaidi ya Haniyah
Aug 17, 2024 23:29Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu ina haki ya kujibu kwa njia halali kitendo cha utawala wa Kizayuni wa Israel cha kumuua kigaidi Ismail Haniyah, aliyekuwa Kiongozi wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas akiwa ziarani hapa mjini Tehran.