-
Netanyahu atangaza kuidhinisha mauzo ya 'kihistoria' ya gesi ya dola bilioni 35 kwa Misri
Dec 19, 2025 03:24Waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel, Benjamin Netanyahu ametangaza kuwa, serikali yake imeidhinisha makubaliano makubwa ya uuzaji wa gesi asilia kwa Misri yenye thamani ya karibu dola bilioni 35, akielezea kwamba makubaliano hayo ni makubwa zaidi katika historia ya Israel kwa upande wa thamani na ujazo wa usafirishaji nje.
-
ICC yatupilia mbali rufaa ya Israel ya kuomba waranti wa kumkamata Netanyahu ubatilishwe
Dec 16, 2025 03:27Kitengo cha rufani cha Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC kimetupilia mbali hoja za utawala wa kizayuni wa Israel za kupinga uhalali wa uchunguzi wa mahakama hiyo kuhusu jinai zilizofanywa Ukanda wa Ghaza kufuatia vita vya kinyama na vya mauaji ya kimbari ambavyo utawala huo haramu ulivianzisha Oktoba 7, 2023 dhidi ya Wapalestina wa ukanda huo uliowekewa mzingiro.
-
Netanyahu: Israel haitaondoka katika maeneo ya kusini ya Syria iliyoyavamia
Dec 08, 2025 06:30Waziri Mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu amesema, jeshi la utawala huo halitaondoka katika maeneo liliyoyavamia na kuyakalia kwa mabavu ya kusini mwa Syria.
-
Haaretz: Netanyahu amepelekea Israel kushindwa katika pande zote, hususan dhidi ya Iran
Nov 26, 2025 12:18"Sera za waziri mkuu Benjamin Netanyahu zimepelekea kushindwa Israel katika pande zote za kidiplomasia, kijeshi, na kimkakati, hususan dhidi ya Iran". Hayo ni kwa mujibu wa Haaretz, gazeti la Israel linalochapishwa kwa lugha ya Kiebrania.
-
Gazeti la Haaretz lamuonya Netanyahu: Israel inaelekea kuporomoka kwa ndani
Nov 26, 2025 03:02Gazeti la Kiebrania la Haaretz limeikosoa serikali ya utawala wa kizayuni wa Israel na waziri mkuu wake Benjamin Netanyahu, likionya kwamba utawala huo unaelekea kuporomoka kwa ndani huku Netanyahu akifanya juu chini ili kuanzisha vita vipya kwa ajili ya eti kuzuia kile gazeti hilo linachokiita "uangamiaji wa Israel".
-
Mamdani: Ikiwa Netanyahu atakuja New York katika mkutano ujao wa UNGA nitaamuru akamatwe
Nov 17, 2025 10:49Meya Mteule wa jiji la New York Zohran Kwame Mamdani ameambia televisheni ya ABC News kwamba atatoa hati ya kukamatwa waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel, Benjamin Netanyahu endapo ataingia ndani ya ardhi ya Marekani mwaka ujao kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
-
Mshindi wa Tuzo ya Nobel ampongeza Netanyahu kwa vita dhidi ya Gaza
Oct 19, 2025 06:32María Corina Machado, kiongozi wa upinzani wa Venezuela na Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel ametoa shukrani zake za dhati kwa Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu kwa maamuzi yake 'magumu' wakati wa vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza.
-
ICC yatupilia mbali rufaa ya Israel dhidi ya hati za kutiwa nguvuni Netanyahu na Gallant
Oct 19, 2025 02:41Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imekataa ombi la utawala wa kizayuni wa Israel la kukata rufaa dhidi ya hati za kukamatwa waziri mkuu wake Benjamin Netanyahu na aliyekuwa waziri wa vita wa utawala huo ghasibu Yoav Gallant kuhusiana na mauaji ya kimbari yaliyofanywa na jeshi la kizayuni katika Ukanda wa Ghaza.
-
Netanyahu ndiye aliyeamuru kushambuliwa kwa droni meli za msafara wa Sumud bandarini Tunisia
Oct 06, 2025 02:22Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa, waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu ndiye aliyetoa idhini ya kufanywa mashambulio ya ndege zisizo na rubani yaliyolenga msafara wa kimataifa wa meli za misaada ya kibinadamu kwa ajili ya Ghaza zilizokuwa zimetia nanga kwenye bandari ya Tunisia.
-
Netanyahu aiomba US iishinikize Misri ipunguze kujiimarisha kijeshi kwenye Peninsula ya Sinai
Sep 21, 2025 09:10Waziri Mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu ameiomba serikali ya Marekani iishinikize Misri ipunguze hatua za kujizatiti kijeshi katika eneo la Peninsula ya Sinai. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa jana Jumamosi na tovuti ya habari ya nchini Marekani ya Axios.