-
Seneta wa Nigeria: Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, nembo ya uhuru duniani
Feb 04, 2026 06:54Seneta Shehu Sani wa Nigeria ambaye pia ni mkuu wa Jukwaa la Haki za Kiraia la Nigeria (CRCN), amesema Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ya mwaka 1979 ni vuguvugu la mwamko wa kihistoria dhidi ya dhulma na ubeberu wa maajinabi, akiyaelezea mapinduzi hayo kama kigezo cha mataifa yanayokandamizwa duniani kote.
-
Nigeria yawafungulia mashtaka watu 9 kwa mauaji ya watu 150 mwaka jana huko Yelwata
Feb 03, 2026 04:37Waendesha mashtaka wamewafungulia mashtaka watu tisa kwa makosa ya ugaidi kuhusiana na moja ya mauaji mabaya zaidi yaliyojiri jimbo la Benue mnamo mwezi Juni mwaka jana. Mauaji hayo yalilenga pakubwa jamii ya Yelwata.
-
Milio ya risasi yasikika mapema leo karibu na uwanja wa ndege wa mji mkuu wa Niger
Jan 29, 2026 09:03Milio ya risasi ilisikika mapema leo karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa katika mji mkuu wa Niger, Niamey kabla ya hali ya utulivu kurejea.
-
Wanajeshi 8 wa Nigeria wauawa katika shambulio la Boko Haram Borno
Jan 22, 2026 02:32Wanajeshi wanane wa Nigeria wameuawa huku wengine 50 wakijeruhiwa baada ya wapiganaji wa genge la kigaidi la Boko Haram kushambulia kambi ya kijeshi katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa nchi.
-
Nigeria yauwa magaidi 40 wa Boko Haram katika operesheni za anga
Jan 19, 2026 08:04Jeshi la Anga la Nigeria limetangaza kuwua limeuwa takriban magaidi 40 wa Boko Haram katika mashambulizi ya anga mtawalia iliyofanya mapema wiki hii katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Mwanachuoni Nigeria: Israel itafutwa katika uso wa dunia ikiishambulia tena Iran
Jan 08, 2026 02:38Mwanachuoni mashuhuri wa Kiislamu wa kaskazini mashariki mwa Nigeria amezionya Israel na Marekani dhidi ya kufanya mashambulizi yoyote ya kijeshi dhidi ya Iran, akisema matokeo yake yatakuwa mabaya zaidi kuliko yale ya vita vya siku 12 vya mwezi Juni mwaka uliopita 2025, na kuilazimisha Israel kuomba usitishaji vita.
-
Magaidi washambulia soko katika jimbo la Niger, Nigeria na kuuwa watu wasiopungua 50
Jan 05, 2026 04:25Polisi wa Nigeria wameripoti kuwa watu wasiopungua 50 wameuawa katika shambulio lililofanywa na magaidi wenye silaha katika soko la kijiji katika Wilaya ya Kabe, eneo la Serikali ya Mtaa ya Borgu katika Jimbo la Niger.
-
Trump asema US imeshambulia kijeshi ndani ya Nigeria kuwalenga wanaoua wakristo wasio na hatia
Dec 26, 2025 04:01Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuwa jeshi la nchi hiyo limefanya shambulio la anga dhidi ya wapiganaji wa kundi la DAESH (ISIS) au ISIL kaskazini magharibi mwa Nigeria.
-
UN yalaani vikali shambulio la kigaidi lililoua waumini msikitini jimboni Borno, Nigeria
Dec 25, 2025 23:53Umoja wa Mataifa umelaani vikali shambulio la kigaidi lililotokea kwenye msikiti ulioko katika Soko la Gamboru, mjini Maiduguri, katika Jimbo la Borno kaskazini-mashariki mwa Nigeria, lililopelekea kuuawa na kujeruhiwa makumi ya Waislamu waliokuwemo msikitini humo.
-
40 wauawa, kujeruhiwa katika shambulio la bomu Msikitini Maiduguri, Nigeria
Dec 25, 2025 02:13Mripuko mkubwa wa bomu umeripotiwa kutikisa Msikiti mmoja wakati wa Swala ya Magharibi usiku wa kuamkia leo huko mjini Maiduguri, makao makuu ya jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria.