Nov 12, 2020 08:02
Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Taasisi za Kimataifa zenye makao yao mjini Vienna Austria amesema ripoti mpya iliyotolewa na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA) inaonyesha kuwa taasisi hiyo ya kimataifa inaendelea kukagua na kufanyia uhakiki miradi ya nyuklia ya Iran bila vizingiti vyovyote.