-
"Kuuawa viongozi wa Muqawama kunaimarisha irada ya Wapalestina"
Jun 09, 2025 02:49Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina imelaani vikali mauaji ya Israel dhidi ya afisa mashuhuri wa Muqawama na watu wengine 30 katika mji wa Gaza na kusisitiza kuwa, mauaji hayo yanayolenga viongozi wa mrengo wa mapambano kamwe hayatadhoofisha uthabiti na azma ya wananchi wa Palestina.
-
Kwa nini mashinikizo dhidi ya Netanyahu hayafanyi kazi?
Jun 04, 2025 11:02Mauaji ya Wapalestina wanaoishi Gaza yanayofanywa na utawala wa Kizayuni yangali yanaendelea, huku nchi na jumuiya mbalimbali za kimataifa zikitoa wito wa kukomeshwa mauaji hayo mara moja.
-
Israel yamjibu Macron: Kutambuliwa Palestina kutasalia kwenye karatasi tu
May 31, 2025 02:22Waziri wa Vita wa Israel, Israel Katz amemsuta na kumkejeli Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ambaye alisema mapema jana kwamba, kutambuliwa kwa taifa la Palestina, kwa masharti, ni "wajibu wa kimaadili."
-
Ben Gvir alitaka jeshi la Israel litumie 'nguvu kamili' Gaza
May 31, 2025 02:22Waziri wa usalama wa ndani wa utawala wa Kizayuni wa Israel mwenye misimamo ya kufurutu ada, Itamar Ben Gvir ametoa wito wa kutumiwa "nguvu kamili" huko Gaza, baada ya madai ya uongo kwamba Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imepinga pendekezo jipya la Marekani kuhusu usitishaji vita.
-
Siku 600 za mauaji ya kimbari Gaza; Hamas yaitisha maandamano
May 28, 2025 06:51Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetoa wito kwa Wapalestina, Waarabu, Waislamu na watu huru kote duniani kushiriki katika harakati ya kimataifa na maandamano ya 'ghadhabu za kimataifa' kuadhimisha siku 600 za "mauaji ya halaiki na njaa" dhidi ya watu wa Gaza.
-
Iran: Israel iliundwa kwa damu; mauaji ya kimbari lazima yakomeshwe sasa
May 16, 2025 07:22Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa taarifa kwa mnasaba wa Siku ya Nakba na kusema kwamba, utawala wa Kizayuni wa Israel "uliasisiwa katika msingi wa umwagaji damu" na kwamba jamii ya kimataifa ina wajibu wa kukomesha mauaji ya kimbari yanayoendelea huko Gaza.
-
Ansarullah: Iran imetekeleza wajibu wake wa Kiislamu kuiunga mkono Palestina
May 16, 2025 06:52Kiongozi wa Harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen ameipongeza Iran kwa uungaji mkono wake usio na kikomo kwa taifa la Palestina na kadhia yao halali na kueleza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu inafuata njia ya heshima katika suala hilo na nchi nyingine zote za Kiislamu lazima zifuate mkondo huo.
-
Shambulio la 3 la kombora la hypersonic la Yemen dhidi ya Ben Gurion
May 14, 2025 11:31Vikosi vya Wanajeshi wa Yemen wamefanya shambulio jipya la kombora la hypersonic dhidi ya utawala haramu wa Israel na kupelekea sauti za ving'ora vya tahadhari kuhanikiza katika sehemu ya kaskazini ya ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na utawala huo pandikizi.
-
Iran yailaani Israel kwa kupiga mabomu kambi za wakimbizi Palestina
May 14, 2025 02:47Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali mashambulizi ya hivi karibuni ya anga dhidi ya kambi za wakimbizi wa Kipalestina yaliyofanywa na utawala ghasibu wa Israel na kusababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa makumi ya Wapalestina wasio na hatia wakiwemo watoto wadogo.
-
Wamorocco: Mgogoro wa kibinadamu Gaza unatisha
May 12, 2025 11:12Wananchi wa Morocco wameandamana kuunga mkono Wapalestina wanaoishi katika Ukanda wa Gaza, wakitangaza mshikamano wao na watoto wa eneo hilo la Palestina lililozingirwa ambao wanakabiliwa na njaa, kiu na maradhi; huku mgogoro mbaya wa kibinadamu uliosababishwa na Wazayuni ukiendelea kuwasakama.