-
Hamas yawataka Wapalestina wajitayarishe kuutetea Msikiti wa al Aqsa
Oct 09, 2021 04:26Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imewataka Wapalestina wajitayarishe kwa ajili ya kuutetea Msikiti wa al Aqsa bila ya kujali uamuzi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kusitisha azma yake ya kuruhusu ibada ya Mayahudi katika eneo hilo tukufu.
-
Wanamapambano Palestina walaani kuvunjiwa heshima Msikiti wa al Aqsa
Oct 08, 2021 13:22Makundi ya mapambano ya ukombozi wa Palestina yametangaza kuwa, kuwaruhusu Wayahudi kufanya ibada katika viwanja vya Msikiti wa al Aqsa ni hatua hatari sana inayovunjia heshima matukufu ya Kiislamu.
-
Az-Zahar: Uingereza ndio iliyoandaa mazingira ya Palestina kuvamiwa na kukaliwa kwa mabavu na Wazayuni
Oct 07, 2021 01:06Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema, wavamizi wa Kiingereza ndio walioandaa mazingira kwa Wazayuni kuvamia na kuikalia kwa mabavu ardhi ya Palestina.
-
"Kujipendekeza Abbas kwa Israel kunaashiria kudidimia Mamlaka ya Ndani Palestina"
Oct 05, 2021 04:30Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imekosoa vikali hatua ya Mamhoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ya kujidhalilisha na kuwaangukia miguuni maafisa wa utawala wa Kizayuni wa Israel na kusisitiza kuwa, kitendo hicho kinaonesha namna mamlaka hiyo inavyoendelea kudidimia na kusambaratika.
-
Abbas akutana na mawaziri wa Israel usiku wa manane Ramallah
Oct 04, 2021 08:07Mamhoumd Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amekutana na kufanya mazungumzo na mawaziri wawili wa utawala haramu wa Israel mjini Ramallah, eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Miaka 21 baada ya Oktoba Mosi 2000; ibra na mazingatio ya Intifadha ya al-Aqswa kwa Wapalestina
Oct 02, 2021 08:22Wananchi wa Palestina wamefanya maandamano kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 21 ya Intifadha ya Quds ambapo wakiwa wamebeba mabango na maberamu wametoa nara za kulaani siasa na jinai za utawala vamizi wa Quds.
-
Maelfu ya Wapalestina wasali Sala ya Ijumaa Quds licha hatua kali za Israel za kuwazuia
Oct 01, 2021 23:05Wapalestina wapatao 50,000 jana walisali Sala ya Ijumaa katika msikiti mtakatifu wa al-Aqswa licha ya hatua kali za jeshi la utawala haramu wa Israel la kuwazuia waumini kuingia katika kibla hicho cha kwanza chah Waislamu.
-
Balozi wa Palestina UN: Israel inapanua kwa siri mpango wake wa silaha za nyuklia
Sep 30, 2021 00:13Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel umekuwa ukipanua kwa siri mpango wake wa silaha za nyuklia na unafanya njama za kukwamisha uhudi za kupatikana eneo lisilo na silaha za nyuklia Asia Magharibi.
-
HAMAS yaishukuru tena Iraq kwa misimamo yake ya kupinga kuanzishwa mapatano na Israel
Sep 27, 2021 22:56Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS kwa mara nyingine tena imeishukuru serikali, makundi ya kisiasa, wazee wa koo na viongozi wa makabila ya Iraq, kwa msimamo wao wa kupinga kuanzishwa mapatano na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
-
Jihadul Islami yatoa onyo kali baada ya Israel kuwaua Wapalestina watano
Sep 27, 2021 04:01Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina imetoa onyo kali kwa utawala wa Kizayuni wa Israel baada ya utawala huo katili kuwaua shahidi wanamapambano watano wa Palestina.