-
Palestina yataka kuharakishwa kufuatiliwa jinai za kivita za Israel
Feb 15, 2021 04:21Wizara ya Mambo ya Nje ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina jana usiku ilitoa tamko na kutaka kuharakishwa kufuatiliwa jinai za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina.
-
UN: Uamuzi wa ICC umefungua mlango wa kupata haki Wapalestina
Feb 10, 2021 20:05Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia masuala ya haki za binadamu katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu amesema uamuzi wa hivi karibuni wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC wa kubariki kuchunguzwa jinai za utawala wa kigaidi wa Israel dhidi ya taifa la Palestina umefungua mlango wa kupata haki Wapalestina.
-
EU yapinga bomoabomoa ya nyumba za raia wa Palestina inayofanywa na Israel
Feb 10, 2021 03:33Msemaji wa Mkuu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya (EU) ametoa taarifa akipinga vikali operesheni ya kuboa nyumba za raia wa Palestina inayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Uamuzi wa ICC; ushindi kwa Wapalestina
Feb 07, 2021 23:22Kufuatia ombi la Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina kwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC kwa ajili ya kuchunguza jinai za utawala wa kigaidi wa Israel dhidi ya taifa la Palestina, majaji wa mahakama hiyo wametoa uamuzi wakisema kuwa mahakama hiyo inafaa kisheria kuchunguza jinai za kivita katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na utawala huo.
-
Imarati, Bahrain zawakatia Wapalestina misaada baada ya kuikumbatia Israel
Feb 07, 2021 04:18Umoja wa Falme za Kiarabu na Bahrain zimepunguza kwa kiasi kikubwa misaada yao ya kifedha iliyokuwa ikiwapa wananchi wa Palestina, baada ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Hamas, Arab League zakaribisha uamuzi wa ICC dhidi ya Israel
Feb 07, 2021 03:48Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imepongeza hukumu ya hivi karibuni ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC yenye maslahi kwa wananchi wa Palestina na iliyoughadhabisha mno utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Netanyahu ahamakishwa na hukumu ya mahakama ya ICC
Feb 06, 2021 04:07Benjamin Netanyahu, waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel ameshindwa kuficha hamaki zake baada ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC kutoa hukumu kwa manufaa ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Wazayuni.
-
Msimamo wa Uturuki baada ya kutiwa saini mapatano kati ya Kosovo na Israel
Feb 05, 2021 06:46Katika hatua inayopaswa kutiliwa maanani, serikali ya Uturuki imepinga kitendo cha kutiwa saini mapatano kati ya Kosovo na utawala wa kibaguzi wa Israel kwa ajili ya kufungua ubalozi wa nchi hiyo katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Polisi wa utawala wa Kizayuni wawaua shahidi kwa kuwapiga risasi vijana wawili Wapalestina
Feb 02, 2021 04:02Polisi wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel wamewaua shahidi kwa kuwapiga risasi vijana wawili Wapalestina baada ya kuvamia eneo moja katika mji Tamra kaskazini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Ukosoaji wa kuchelewa wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kuhusu kadhia ya Palestina
Jan 29, 2021 23:14Akizungumza Jumanne katika kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kilichoandaliwa kwa ajili ya kujadili masuala ya eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati) Ahmad Abu al-Ghait, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu au kwa jina jingine Arab League, alisema kuwa Wapalestina wamepitia mashinikizo makubwa yasiyo na mfano wake katika miaka minne ya utawala wa rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump.