-
Makundi ya ukombozi ya Palestina yajitayarisha kukabiliana na Wazayuni Ukanda wa Gaza
Mar 13, 2020 23:02Kutokana na kuongezeka uwezekano wa utawala wa Kizayuni wa Israel kushambulia eneo la Ukanda wa Gaza, makundi ya mapambano ya ukombozi wa Palestina yamejiweka katika hali ya tahadhari kwa ajili ya kukabiliana na hujuma ya aina yoyote ya utawala huo haramu.
-
Marekani yatekeleza njama mpya dhidi ya Wapalestina kwa kubadilisha utambulisho wa wakazi wa Quds
Mar 12, 2020 12:03Harakati ya Kidemokrasia kwa ajili ya Ukombozi wa Palestina imesema, hatua ya wizara ya mambo ya nje ya Marekani ya kubadilisha utambulisho wa Wapalestina wa eneo la Baitul Muqaddas Mashariki ni hujuma ya dhahiri na uchokozi wa wazi dhidi ya utambulisho wa Wapalestina.
-
Palestina yaionya Israel dhidi ya kutumia vibaya suala la virusi vya Corona
Mar 11, 2020 08:28Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina imewatahadharisha Wazayuni kutotumia vibaya suala la virusi vya Corona kuzishughulisha fikra za walimwengu ili wapate fursa ya kupora ardhi zilizosalia za Palestina.
-
HAMAS yatupilia mbali ombi la Marekani la kuweko uhusiano wa kidiplomasia baina yao
Mar 03, 2020 08:20Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina HAMAS ametupilia mbali ombi la Marekani la kutaka Washingto iwe na uhusiano wa kisiasa na harakati hiyo ya Kiislamu.
-
Baraza la Mamufti Russia lamshukuru Kiongozi Muadhamu kwa kuwatetea Wapalestina
Mar 01, 2020 04:39Baraza la Mamufti la Russia limempongeza na kumshukuru Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei kwa kutetea haki halali za Wapalestina.
-
EU yakosoa mpango wa Israel wa kujenga vitongoji vipya Ukingo wa Magharibi
Feb 29, 2020 09:50Umoja wa Ulaya umekosoa vikali mpango wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kujenga maelfu ya vitongoji vipya vya walowezi wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu na utawala huo ghasibu.
-
Risasi za jeshi la Israel zawapofusha Wapalestina 21 Ukanda wa Gaza
Feb 27, 2020 09:41Kituo cha Haki za Binadamu cha Beytulahm (Bethlehem) huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu kimeripoti kuwa, Wapelestina 21 katika Ukanda wa Gaza wamesababishiwa upofu na ufyatuaji risasi wa jeshi katili la utawala wa Kizayuni wa Israel ndani ya miaka miwili iliyopita.
-
Baraza la Usalama la UN launga mkono suala la kuundwa nchi huru ya Palestina
Feb 26, 2020 01:03Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetangaza uungaji mkono wake kamili kwa suala la kuundwa nchi huru ya Palestina na kuendelezwa "mazungumzo yenye itibari" baina ya pande mbili.
-
Utawala wa Kizayuni watishia kuwaua kigaidi viongozi wa Palestina huko Ukanda wa Ghaza
Feb 25, 2020 10:02Viongozi wa utawala wa Kizayuni wametishia kuwaua kigaidi viongozi wa Harakati za Muqawama wa Kiislamu za Palestina za Hamas na Jihadul Islami huko Ukanda wa Ghaza.
-
Rais wa Tunisia: Quds ni mji mkuu wa Palestina, si bidhaa ya kuuzwa
Feb 25, 2020 04:18Rais Kais Saied wa Tunisia amesema Palestina ni milki ya Wapalestina na Quds tukufu inapaswa kuwa mji mkuu wa taifa hilo la Kiarabu.