-
Uingereza yalaumiwa kwa kuzuia kutangazwa ukweli kuhusu Palestina
Aug 19, 2018 23:24Zaidi ya mashirika 80 yanayojishughulisha na masuala haki za watu weusi na watu wenye asili ya Asia pamoja na jamii ya wachache nchini Uingereza yamesema kuwa, kuna njama za makusudi zinafanyika nchini humo kuzuia kujadiliwa na kuwekwa wazi kadhia ya Palestina.
-
Mapatano ya kitaifa; ngao ya Wapalestina mkabala na njama ya "Muamala wa Karne"
Aug 18, 2018 11:10Khalid Mash'al Mkuu wa zamani wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesisitiza kuwa muafaka wa kitaifa baina ya Wapalestina ni kama ngao ya muqawama katika kukabiliana na njama ya "Muamala wa Karne."
-
UN yatoa mapendekezo ya kuboresha hali ya Wapalestina
Aug 18, 2018 10:00Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa mapendekezo kadhaa ya kuwasaidia watu wa Palestina katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na Israel.
-
Silaha ya Muqawama; wenzo wa kuwahami wananchi wa Palestina
Aug 13, 2018 03:00Khalid al-Batsh, kiongozi mwandamizi wa harakati ya Jihadul Islami ya Palestina amesisitiza kuwa silaha ya Muqawama ndio wenzo wa kulihami taifa na wananchi wa Palestina dhidi ya Wazayuni maghasibu.
-
Algeria yalaani jinai za wanajeshi wa Israel katika Ukanda wa Ghaza
Aug 11, 2018 22:39Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Algeria amelaani vikali jinai za wanajeshi makatili wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza.
-
Wazayuni wachochea vita zaidi dhidi ya Wapalestina
Aug 09, 2018 23:20Licha ya kuweko onyo la kimataifa kwa utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu jinai zake dhidi ya Wapalestina, baraza la mawaziri la utawala huo dhalimu jana usiku liliitisha kikao maalumu na kutaka mashambulizi dhidi ya wananchi wa Ghaza yaendelee.
-
Jihadul Islami: Saudia na Imarati zinashirikiana na Marekani kuikandamiza Palestina
Aug 08, 2018 23:55Mwakilishi wa harakati ya Jihad al Islami ya Palestina nchini Iran amesema kuwa, Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati), zinashiriki waziwazi katika 'Mapatano ya Karne' ambayo yameandaliwa na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kuliangamiza taifa la Palestina
-
Udharura wa kuundwa kambi ya kimataifa dhidi ya sheria ya kibaguzi ya 'Nchi ya Mayahudi pekee'
Jul 30, 2018 03:45Ismail Haniya, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amemuandika barua Mahathir Muhammad Waziri Mkuu wa Malaysia akitaka kuweko harakati za kweli na athirifu katika Ulimwengu wa Kiislamu na jamii ya kimataifa kwa ajili ya kulaani sheria mpya ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya 'Nchi ya Mayahudi Pekee' na kuzuia kutekelezwa sheria hiyo.
-
Saudia yawapiga marufuku mahujaji kujadili masuala ya Yemen na Palestina
Jul 28, 2018 06:52Kufuatia kushindwa siasa za Saudia kuanzia nchini Syria, Iraq na Yemen, na kadhalika kashfa za kuyasaidia kifedha makundi ya kigaidi na Kiwahabi, serikali ya Riyadh imepiga marufuku vikao vya aina yoyote vinavyojadili masuala ya kisiasa yakiwemo masuala ya Yemen na Palestina.
-
Palestina yateuliwa kuongoza Kundi la 77 la UN
Jul 27, 2018 03:36Palestina imeteuliwa kuwa mwenyekiti wa kiduru wa Kundi la 77 (G77) linalojihusisha na masuala ya uchumi wa nchi zinazostawi, ambazo zinaunda asilimia 80 ya idadi ya watu wote duniani.