-
Waandamanaji Uturuki: Marekani ndiye shetani halisi
Jan 01, 2024 08:25Kwa mara nyingine tena, wananchi wa Uturuki wamekusanyika nje ya Ubalozi Mdogo wa Marekani mjini Istanbul katika maandamano ya kuonyesha himaya na uungaji mkono wao kwa wananchi wa Palestina hususan wa Ukanda wa Gaza wanaoendelea kukabiliwa na hujuma na mashambulio ya kinyama ya utawala haramu wa Israel.
-
Maandamano ya waungaji mkono wa Palestina mbele ya Jengo la Biashara la Kimataifa la Marekani
Dec 31, 2023 04:39Waungaji mkono wa wananchi madhulumu wa Palestina wamekusanyika mbele ya Jengo la Biashara la Kimataifa la Marekani wakipinga siasa za serikali ya Marekani za kutoa himaya kwa mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Ansarullah: Vikosi vya Yemen vina 'hamu' ya kukabiliana na US Bahari Nyekundu
Dec 30, 2023 06:55Afisa mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Ansarullah ya Yemen amesema vikosi vya jeshi la nchi hiyo vipo tayari kuingia katika makabiliano ya kijeshi na Marekani iwapo hali ya taharuki itashtadi katika Bahari Nyekundu.
-
UNICEF: Idadi ya watoto Wapalestina waliouliwa na Israel Ukingo wa Magharibi pia haijawahi kushuhudiwa
Dec 29, 2023 05:57Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF kanda ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini amesema, idadi ya watoto Wapalestina waliouliwa na askari wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel katika mwaka huu huko Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na Baitul Muqaddas Mashariki ni kubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa kwa kila mwaka katika eneo hilo.
-
Jihadul Islami yaiambia Israel: Subirini jibu letu kwa mauaji ya mshauri wa IRGC
Dec 26, 2023 23:24Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina sanjari na kulaani mauaji ya Kamanda Sayyid Razi Mousavi, aliyekuwa mshauri wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) imesisitiza kuwa, utawala wa Kizayuni unapasa kusubiri jibu kali na zito kwa kitendo chake hicho cha kioga.
-
Maelfu washiriki kwenye maandamano ya Morocco ya kuunga mkono Palestina
Dec 25, 2023 03:00Maelfu ya watu nchini Morocco wamefanya mojawapo ya maandamano makubwa zaidi ya kuunga mkono Palestina mjini Rabat, tangu kuzuka kwa vita vya Gaza, wakati wakiitisha kuvunjwa kwa mahusiano kati ya taifa lao na Israel.
-
Ebrahim Raisi: Wanaodai kuwa wafuasi wa Nabii Issa (as) hawapaswi kuiunga mkono Israel na mauaji yake dhidi ya watoto
Dec 25, 2023 00:57Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, kuwa, wale wote wanaodai kwamba ni wafuasi wa Nabii Issa Masih (as) hawapaswi kuiunga mkono Israel na mauaji yake dhidi ya watoto huko katika Ukanda wa Gaza.
-
Mwakilishi wa Jihadul Islami: Iran ni muungaji mkono pekee wa wananchi wa Gaza na wanaodhulumiwa duniani
Dec 24, 2023 23:12Mwakilishi wa Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina nchini Iran amekosoa kimya cha nchi za Magharibi mkabala wa vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya wananchi wa Palestina katika Ukanda wa Gaza na kusema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni muungaji mkono pekee wa wanaodhulumiwa duniani.
-
Al-Wefaq: Bahrain imewasaliti Wapalestina kwa kujiunga na muungano wa US
Dec 22, 2023 22:57Chama kikuu cha upinzani nchini Bahrain cha al-Wefaq kimesema hatua ya utawala wa Aal-Khalifa ya kujiunga na muungano wa baharini wa Marekani katika Bahari Nyekundu ni kusaliti kadhia ya Palestina.
-
Msaada wa Marekani kwa Israel watajwa kuwa sababu kuu ya jinai dhidi ya Wapalestina
Dec 22, 2023 04:37Washiriki katika mkutano wa mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (PUIC) wamesisitiza kuwa misaada na uungaji mkono wa Marekani kwa utawala wa Kizayuni wa Israel ndio sababu kuu ya kuendelea jinai dhidi ya wananchi wa Palestina.