-
Marekani kuuhamishia Quds (Jerusalem) ubalozi wake wa Tel Aviv mwezi Mei mwaka huu
Feb 24, 2018 00:28Licha ya upinzani mkubwa ulioanzia eneo la Mashariki ya Kati na ulimwengu kwa jumla, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imetangaza kuwa mnamo mwezi Mei mwaka huu ubalozi wa nchi hiyo ulioko Tel Aviv utahamishiwa Baitul Muqaddas inayokaliwa kwa mabavu.
-
Njama za utawala wa Kizayuni wa Israel za kuwatimua Wakristo kutoka Quds Tukufu
Feb 04, 2018 04:36Baraza la Kiislamu-Kikristo la Kuunga Mkono Quds Tukufu (Jerusalem) limetangaza kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel unatekeleza njama za kuwatimua Wakristo kutoka Quds ili kubadilisha muundo wa kijamii wa mji huo uwe ni aghalabu wa Mayahudi.
-
Arab League: Hujuma dhidi ya Beitul-Muqaddas ni kucheza na moto
Feb 02, 2018 00:49Ahmed Aboul Gheit, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu amesema kuwa, hujuma na uvamizi dhidi ya Beitul Muqaddas ni sawa na kucheza na moto.
-
Araqchi: Quds ni mji mkuu wa asili wa Ulimwengu wa Kiislamu
Jan 31, 2018 12:02Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema: Ni yakini kwamba Quds tukufu ni mji mkuu wa asili wa Ulimwengu wa Kiislamu na utarejea mikononi mwa Umma wa Kiislamu.
-
PLO: Hakuna mazungumzo na Marekani bila ya kufutwa uamuzi wa Trump kuhusu Quds
Jan 31, 2018 04:40Katibu wa kamati ya utendaji ya Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) amesisitiza kuwa, hakutafanyika mazungumzo au maonyesho yoyote yale na Marekani madhali Rais Donald Trump wa nchi hiyo hajafuta uamuzi wake wa kuitangaza Beitul-Muqaddas kuwa mji mkuu wa utawala haramu wa Israel.
-
UN yapinga tena uamuzi wa Marekani wa kuhamishia ubalozi wake Quds tukufu
Jan 26, 2018 13:13Kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kimesisitiza tena upinzani wa jamii ya kimataifa dhidi ya uamuzi wa Marekani wa kuhamishia ubalozi wake katika mji mtakatifu wa Quds unaokaliwa kwa mabavu na Israel.
-
Baraza la Usalama linakutana leo kujadili kadhia ya Palestina
Jan 25, 2018 03:18Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linakutana leo Alkhamisi katika kikao chake cha dharura kwa shabaha ya kujadili kadhia ya Palestina.
-
Mkutano wa al-Azhar: Baytul-Muqaddas ni mji mkuu wa milele wa Palestina
Jan 19, 2018 00:44Washiriki wa mkutano wa kimataifa wa kuunga mkono Quds uliofanyika katika Chuo Kikuu cha al-Azhar huko Cairo Misri umesisitiza umuhimu wa kutangazwa Baytul-Muqaddas kuwa mji mkuu wa milele wa Palestina.
-
Abbas: Quds inaweza kuwa lango la amani au vita, Trump achague
Jan 17, 2018 23:03Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina, Mahmoud Abbas amesema mji wa Baitul Muqaddad unaweza kuwa lango la kupatikana amani au kuibua vita, na Marekani ina khiari ya kuchagua njia inayoitaka.
-
Kiongozi Muadhamu: "Ufidhuli mkubwa inaofanya Marekani" kuhusiana na Quds Tukufu hautafika popote
Jan 16, 2018 13:39Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Marekani imekuwa ikifanya "ufidhuli mkubwa" kuhusu Quds Tukufu na kuongeza kuwa njama zake hizo hazitafika popote.