Dec 15, 2023 02:56
Bunge la wawakilishi la Marekani jana Jumatano lilipasisha azimio kwa kura 221 za ndio mkabala wa 212 za kupinga kuanzisha rasmi uchunguzi wa kumsaili Rais Joe Biden wa nchi hiyo. Kabla ya kura hiyo, Kelly Armstrong, Mwakilishi wa Kongresi ya Marekani kwa niaba ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Marekani, alichapisha rasimu ya azimio kwa ajili ya kuendelea uchunguzi huo tajwa kwa lengo la kumuuzulu Rais Joe Biden wa Marekani.