-
Sunak: Safari za kwanza za ndege kuelekea Rwanda za wanaotafuta hifadhi zitaanza baada ya wiki 10 hadi 12
Apr 22, 2024 23:38Waziri Mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak, ameahidi kwamba safari za kwanza za ndege za nchi hiyo za raia wa nchi mbalimbali wanaotafuta hifadhi zitaanza kuondoka Uingereza kuelekea Rwanda baada ya wiki 10-12.
-
Kagame ailaumu jamii ya kimataifa kwa kutochukua hatua za kuzuia mauaji ya kimbari ya Rwanda
Apr 07, 2024 23:09Rais Paul Kagame wa Rwanda ameilaumu jamii ya kimataifa kwa kutochukua hatua za kuzuia mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 nchini humo. Rais Kagame alibainisha haya jana wakati Wanyarwanda walipoadhimisha miaka 30 tangu kujiri mauaji hayo ya kutisha ambapo Wahutu wenye misimamo mikali waliwauwa Watutsi wasiopungua laki nane.
-
Macron: Ufaransa na washirika wake wangeweza kuzuia mauaji ya kimbari ya Rwanda
Apr 05, 2024 04:21Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron jana Alhamisi alieleza kuwa Ufaransa na washirika wake wangeweza kukomesha mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 lakini hawakuwa na nia ya kufanya hivyo. Weledi wa mambo wametaja matamshi haya ya Macron kuwa tangazo kali la kuungama kabla ya Rwanda kuadhimisha kutimia miaka 30 tangu nchi hiyo ikumbwe na mauaji ya kimbari ambapo Watutsi na wahutu wenye misimamo ya wastani zaidi ya laki nane waliuawa.
-
Kagame: Rwanda haijahusika kivyovyote na mapigano mashariki ya DRC
Jan 24, 2024 00:07Rais wa Rwanda, Paul Kagame amesema nchi hiyo haijahusika kivyovyote na mapigano na ghasia zinazoendelea kushuhudiwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Waziri Mkuu wa UK: Nitapuuza sheria ya kimataifa kuhusu kuwapeleka wahamiaji Rwanda
Jan 20, 2024 00:32Waziri Mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak ameendelea kung'ang'ania mpango wa serikali ya London wa kuhamishia waomba hifadhi nchini Rwanda, akisisitiza kuwa yuko tayari kupuuza sheria ya kimataifa ambayo imezuia kwa muda utekelezaji wa mpango huo tata.
-
Burundi yafunga mpaka wake na Rwanda baada ya shambulio la waasi
Jan 12, 2024 03:50Burundi imetangaza kuwa imefunga mpaka wake na Rwanda kuanzia jana Alkhamisi kwa muda usiojulikana.
-
Rais wa DRC amfananisha Rais Kagame na Adolf Hitler
Dec 09, 2023 23:33Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amemshabihisha mwenzake wa Rwanda, Paul Kagame na mtawala wa zamani wa Ujerumani ya Manazi, Adolf Hitler.
-
Mahakama: Ni kinyume cha sheria kwa UK kuwapeleka Rwanda watafuta hifadhi
Nov 15, 2023 11:26Mahakama ya Juu ya Uingereza imesema mpango wa serikali ya London wa kuwapeleka nchini Rwanda wakimbizi na waomba hifadhi walioko nchini humo unakiuka sheria.
-
Mahakama Kuu Uingereza kutoa uamuzi kuhusu uhalali wa kupelekwa Rwanda waomba hifadhi
Nov 10, 2023 06:15Mahakama Kuu ya Uingereza wiki ijayo itatoa uamuzi iwapo mpango wa serikali ya nchi hiyo wa kuwapeleka nchini Rwanda, wakimbizi na waomba hifadhi walioko nchini humo ni halali au la.
-
Rwanda yapeleka misaada ya kibinadamu Ukanda wa Gaza
Oct 22, 2023 02:56Rwanda imetuma misaada ya kibinadamu Ukanda wa Gaza, kuonyesha mshikamano na wananchi wa Palestina waliohasiriwa na kujeruhiwa katika mashambulio ya kinyama ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel dhidi ya eneo hilo.