-
Israel ilitoa msaada wa kijasusi kwa Saudia katika mauaji ya Khashoggi
Dec 03, 2018 03:19Imebainika kuwa shirika moja la kijasusi la utawala wa Kizayuni wa Israel lilitoa msaada mkubwa kwa ufalme Saudi Arabia ili kufanikisha mauaji ya mwandishi habari Jamal Khashoggi ambaye alikuwa mkosoaji mkubwa wa ufalme huo wa kiimla.
-
Argentina yaanza kufuatilia mashtaka ya Shirika la Haki za Binaadamu (Human Rights Watch) dhidi ya Bin Salman
Nov 29, 2018 09:49Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Argentina ameanza kufuatilia mashtaka ya Shirika la Haki za Binaadamu la Human Rights Watch dhidi ya Mohammad Bin Salman, Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudia kutokana na vitendo vyake vinavyokiuka haki za binaadamu.
-
Sudan inapanga kujitoa kwenye muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudia dhidi ya Yemen
Nov 28, 2018 13:06Duru za kidiplomasia zimeripoti kuwa, umejitokeza mvutano kati ya Saudi Arabia na Sudan kutokana na kubadilika misimamo ya pande mbili juu ya suala la kuendelezwa hujuma na mashambulio ya kijeshi dhidi ya Yemen.
-
Maelfu ya Wapakistan wanashikiliwa katika jela za Saudia na Imarati
Nov 28, 2018 12:34Waziri wa zamani wa Masuala ya Ustawi wa Kieneo katika jimbo la Khyber Pakhtunkhwa nchini Pakistan amefichua kwamba, jumla ya raia 3,309 wa nchi hiyo wanashikiliwa katika jela za Saudi Arabia.
-
Serikali ya Algeria yalaani mauaji ya Khashoggi, upinzani dhidi ya safari ya bin Salman waongezeka
Nov 26, 2018 12:13Huku kukiwa na habari ya uwezekano wa mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia kutembelea Algeria na kuongezeka upinzani wa wananchi wa nchi hiyo dhidi ya ziara hiyo, serikali ya Algiers imelaani rasmi mauaji ya Jamal Ahmad Khashoggi, mwandishi wa habari aliyekuwa akiukosoa utawala wa Aal Saud.
-
Bin Salman baina ya wahka wa ndani na malalamiko ya kimataifa
Nov 26, 2018 01:00Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia Muhammad bin Salman yuko katika safari ya kuzitembelea nchi 6 za Kiarabu na inatazamiwa kuwa, baada ya safari hiyo ataelekea Argentina kushiki mkutano wa G20. Hata hivyo Bin Salman amepatwa na wahka na wasiwasi mkubwa kutokana na uwezekano wa kutokea mapinduzi ndani ya kizazi cha Aal Saud na malalamiko yanayozidi nje ya nchi hiyo.
-
Mujtahid: Kuna uwezekano wa kutokea jambo lisilotarajiwa ndani ya kasri la kifalme nchini Saudi Arabia
Nov 24, 2018 11:33Mwanaharakati maarufu wa mitandao ya kijamii nchini Saudia, Mujtahid amefichua habari ya kuwepo hali isiyo ya kawaida ndani ya kasri la kifalme nchini humo na kwamba kile kinachoendelea hivi sasa ndani ya kasri hilo kinaashiria wasi wasi mkubwa.
-
Mwanahakari ataka kufanywa uchunguzi maalumu katika jela za Saudia
Nov 23, 2018 11:20Kiongozi wa masuala ya Saudi Arabia katika shirika la haki za binaadamu la Human Rights Watch ametaka kufanyike uchunguzi wa kimataifa kuhusiana na hali ya wafungwa nchini humo.
-
Saudia yawazuia watoto wa wapinzani walioko korokoroni wasitoke nje ya nchi
Nov 21, 2018 23:16Mbali na viongozi wa Saudi Arabia kuwashikilia maelfu ya wapinzani na wanaharakati wa kisiasa nchini humo, inawazuia pia watoto wao wasitoke nje ya nchi.
-
Jibu la Iran kuhusu madai ya haki za binadamu ya Saudi Arabia
Nov 20, 2018 00:19Abdullah Al Mualami Mwakilishi wa Saudi Arabia katika kikao cha hivi karibuni cha Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya haki za binadamu alitoa madai yasiyo na msingi dhidi ya Iran.