-
Wasaudia 18 wazuiwa kuingia Ujerumani kwa tuhuma za mauaji ya Khashoggi
Nov 19, 2018 12:10Wizara ya Mambo ya Nje ya Ujerumani imezuia kuingia nchini humo kundi moja la raia wa Saudi Arabia wanaotuhumiwa kuhusika katika mauaji ya mwandishi wa habari Jamal Khashoggi aliyekuwa akiukosoa utawala wa Aal Saud.
-
Umoja wa Ulaya waitaka Saudi Arabia iweke wazi kikamilifu kuhusu mauaji ya Khashoggi
Nov 18, 2018 10:44Mkuu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya ameitaka Saudi Arabia kuweka wazi kikamilifu mauaji ya mwandishi habari mkosoaji wa Saudia.
-
Ujerumani: Maelezo ya Saudi Arabia kuhusu mauaji ya Khashoggi hayakinaishi
Nov 16, 2018 21:41Serikali ya Ujerumani imetangaza kuwa, maelezo yaliyotolewa na Saudi Arabia kuhusu mauaji ya mkosoaji wa utawala wa nchi hiyo, Jamal Khashoggi hayatoshi.
-
Seneti ya Marekani yataka kutouziwa silaha Saudi Arabia
Nov 16, 2018 11:16Kundi la Maseneta wa Marekani limewasilisha muswada unaotaka kupigwa marufuku uuzaji wa silaha za nchi hiyo kwa Saudi Arabia.
-
Marekani yajitoa kimasomaso kwa kuwawekea vikwazo watu waliohusika kumuua Khashoggi
Nov 16, 2018 04:11Wizara ya Hazina ya Marekani na katika hatua yake iliyochelewa, imewawekea vikwazo raia kadhaa wa Saudi Arabia kutokana na mauaji dhidi ya Jamal Khashoggi, mwandishi habari na mkosoaji wa utawala wa Aal-Saud.
-
IRGC: Radiamali ya Iran kwa bwabwaja za Saudia ni ya kimyakimya lakini inayoumiza
Nov 15, 2018 11:57Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH) amesema bwabwaja na matamshi hewa yanayotolewa na utawala wa Aal-Saud dhidi ya Iran hayataishia hivi hivi bila kupata jibu, na kwamba radiamali ya Jamhuri ya Kiislamu kwa vitendo hivyo vya kiuhasama ni ya kimyakimya na ambayo sio ya kimaonesho, lakini inayoumiza.
-
Ripoti: Maelfu ya wasichana wa Burundi wapotezwa Saudi Arabia + Sauti
Nov 13, 2018 05:53Kuna ripoti zinazosema kuwa wanawake na wasichana 4,500 raia wa Burundi wamepelekwa Saudi Arabia na Oman tangu mwaka 2015 katika kile kinachodaiwa na watetezi wa haki za binadamu kuwa ni biashara ya binadamu. Serikali ya Burundi imeitisha mkutano maalumu kujadili suala hilo. Hamida Issa na maelezo zaidi kutoka Bujumbura...
-
Bahram Qassemi: Wananchi wa Iran watazishinda siasa za ubabe na utumiaji mabavu
Nov 11, 2018 04:21Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, wananchi wa Iran wataushinda ubabe na utumiaji mabavu kutoka upande wowote ule, na historia ni ushahidi wa wazi wa utamaduni na mwenendo huu wa Wairani.
-
Pasipoti za utawala wa Kizayuni kutumiwa katika safari ya kuendea Saudi Arabia
Nov 09, 2018 11:04Mtandao mmoja wa habari wa utawala haramu wa Kizayuni umeandika kwamba, hivi karibuni Wazayuni watatumia pasipoti za utawala wa Israel katika safari zao nchini Saudi Arabia.
-
WFP: Mamilioni ya Wayemen watakufa njaa vita vikiendelea
Nov 09, 2018 04:24Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani, WFP, limetahadharisha kuwa iwapo vita havitamalizika Yemen, mamilioni ya Wayemen watakufa njaa.