-
IRGC: Radiamali ya Iran kwa bwabwaja za Saudia ni ya kimyakimya lakini inayoumiza
Nov 15, 2018 11:57Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH) amesema bwabwaja na matamshi hewa yanayotolewa na utawala wa Aal-Saud dhidi ya Iran hayataishia hivi hivi bila kupata jibu, na kwamba radiamali ya Jamhuri ya Kiislamu kwa vitendo hivyo vya kiuhasama ni ya kimyakimya na ambayo sio ya kimaonesho, lakini inayoumiza.
-
Ripoti: Maelfu ya wasichana wa Burundi wapotezwa Saudi Arabia + Sauti
Nov 13, 2018 05:53Kuna ripoti zinazosema kuwa wanawake na wasichana 4,500 raia wa Burundi wamepelekwa Saudi Arabia na Oman tangu mwaka 2015 katika kile kinachodaiwa na watetezi wa haki za binadamu kuwa ni biashara ya binadamu. Serikali ya Burundi imeitisha mkutano maalumu kujadili suala hilo. Hamida Issa na maelezo zaidi kutoka Bujumbura...
-
Bahram Qassemi: Wananchi wa Iran watazishinda siasa za ubabe na utumiaji mabavu
Nov 11, 2018 04:21Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, wananchi wa Iran wataushinda ubabe na utumiaji mabavu kutoka upande wowote ule, na historia ni ushahidi wa wazi wa utamaduni na mwenendo huu wa Wairani.
-
Pasipoti za utawala wa Kizayuni kutumiwa katika safari ya kuendea Saudi Arabia
Nov 09, 2018 11:04Mtandao mmoja wa habari wa utawala haramu wa Kizayuni umeandika kwamba, hivi karibuni Wazayuni watatumia pasipoti za utawala wa Israel katika safari zao nchini Saudi Arabia.
-
WFP: Mamilioni ya Wayemen watakufa njaa vita vikiendelea
Nov 09, 2018 04:24Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani, WFP, limetahadharisha kuwa iwapo vita havitamalizika Yemen, mamilioni ya Wayemen watakufa njaa.
-
"Saudia ilitumia programu ya udukuzi ya Israel kumfuatilia Kashoggi"
Nov 08, 2018 11:49Edward Snowden, afisa wa zamani wa Shirika la Usalama wa Taifa la Marekani (NSA) amefichua nafasi ya utawala haramu wa Israel katika mauaji ya kikatili ya mkosoaji wa utawala wa Saudi Arabia, Jamal Khashoggi yaliyofanywa na Riyadh nchini Uturuki mwezi uliopita.
-
Paris: Upo uwezekano wa kuiwekea vikwazo Saudi Arabia
Oct 31, 2018 21:54Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa amesema kuwa upo uwezekano Saudia ikawekewa vikwazo iwapo itakuwa imehusika katika mauaji ya mwandishi wa habari mkosoaji wa utawala wa ukoo wa Aal Saud, Jamal Khashoggi.
-
Dick Black: Uhusiano wa Marekani na Saudia unaainishwa na fedha
Oct 30, 2018 22:56Richard Hayden Black, Seneta wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa, uhusiano wa Marekani na Saudi Arabia hautegemei misingi ya matukufu ya kimaadili, bali unategemea maslahi ya kiuchumi.
-
L'Express: Vyombo vya ujasusi Uingereza vilijua mapema azma mbaya ya Wasaudi dhidi ya Khashoggi
Oct 29, 2018 10:34Gazeti la kila wili la Kifaransa la L'Express limefichua kuwa, vyombo vya intelijensia vya Uingereza vilikuwa na taarifa kwamba, mmoja wa wanawafalme wa Saudia ametoa amri ya kutekwa na hata kuuawa Jamal Khashoggi, mwandishi habari na mkosoaji wa utawala wa Aal-Saud.
-
"Uingereza ni mshiriki wa jinai za Saudi Arabia nchini Yemen"
Oct 29, 2018 01:08Mbunge mmoja mwandamizi wa Uingereza amesema kuwa serikali ya nchi hiyo ni mshiriki wa jinai za Saudi Arabia dhidi ya wananchi wa Yemen.