-
Malaysia yasimamisha ushirikiano wake wa kijeshi na Saudia katika vita dhidi ya Yemen
Jun 28, 2018 08:52Waziri wa Ulinzi wa Malaysia amesema kuwa, nchi yake imesimamisha ushirikiano wake wa kijeshi na Saudi Arabia katika vita dhidi ya Yemen.
-
Human Rights Watch yafurahishwa na kuingizwa Saudia katika orodha nyeusi ya kuvunja haki za binadamu
Jun 27, 2018 03:27Shirika la kimataifa la Human Rights Watch limepokea kwa furaha hatua ya kuingizwa jina la Saudi Arabia katika orodha nyeusi ya wavunjaji wa haki za watoto wadogo na kusema kuwa hiyo ni hatua muhimu.
-
"Saudia iliipa hongo timu ya taifa ya Misri ikubali kuifunga kombe la dunia" - Mwandishi
Jun 27, 2018 03:25Mwandishi mmoja wa Misri amelalamika kuwa serikali ya nchi yake ilipokea rushwa na hongo kutoka kwa Saudi Arabia na kuilazimisha timu ya taifa ya nchi hiyo ikubali kufungwa na Saudia katika mashindano ya fainali za kombe la dunia yanayoendelea nchini Russia hivi sasa.
-
Njia ya reli ya kuiunganisha Israel na Saudi Arabia iko mbioni kujengwa
Jun 24, 2018 22:25Kanali ya Pili ya televisheni ya Israel imetangaza habari ya kukubaliana Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benajmain Netanyahu na Waziri wa Barabara na Uchukuzi wa utawala huo, Yisrael Katz, kuhusu kuanza ujenzi wa njia ya reli ya kuiunganisha Saudi Arabia na ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Shakhsia tofauti wafanya maandamano London kupinga uungaji mkono wa UK kwa Saudia Yemen
Jun 23, 2018 20:43Kundi la wawakilishi wa bunge, wahadhiri wa vyuo vikuu na watu wenye vipawa tofauti nchini Uingereza, wamefanya maandamano mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo wakilaani uungaji mkono wa serikali ya London kwa uvamizi wa Saudia nchini Yemen.
-
Qatar yataka Saudia na Imarati zitimuliwe Baraza la Haki za Binaadamu
Jun 23, 2018 09:42Baada ya kupita mwaka mmoja tangu kukatwa mahusiano ya nchi za Kiarabu na Qatar na kadhalika kuiwekea vikwazo na mzingiro wa kila upande nchi hiyo, serikali ya Doha imetaka uanachama wa Saudia na Imarati katika Baraza la Haki za Binaadamu usimamishwe.
-
Syria: Riyadh ingali inawazuia raia wetu kwenda kufanya Hija
Jun 23, 2018 02:55Serikali ya Syria imeukosoa vikali utawala wa Aal-Saud kwa kuingiza siasa katika amali tukufu ya Hija, ambapo Riyadh imewazuia raia wa Syria kwenda kutekeleza ibada hiyo kwa mwaka wa saba mfululizo.
-
Jumuiya ya Maimamu Tunisia: Saudia inatumia mapato ya Hija kushambulia nchi za Waislamu
Jun 21, 2018 23:16Jumuiya ya Maimamu wa Swala za Jamaa nchini Tunisia imetoa taarifa ikisisitiza kuwa Saudi Arabia inatumia mapato yanayotokana na ibada ya Hija kwa ajili ya kuzishambulia nchi nyingine za Kiislamu na imemtaka Mufti Mkuu wa nchi hiyo kusimamisha safari za kwenda kutekeleza ibada ya Hija mwaka huu huko Saudia.
-
Ndege za Saudia zadondosha mabomu Hudaydah Yemen wakati wa Sala ya Idul Fitri
Jun 15, 2018 10:59Ndege za kivita za muungano unaoongozwa na Saudia zimedondosha mabomu katika maeneo ya mji wa bandarini ya Hudaydah nchini Yemen wakati wakaazi wa mji huo wakiwa wamekusanyika kwa ajili ya Sala ya Idul Fitr mapema leo asubuhi.
-
Saudia yadondosha mabomu katika kituo cha tiba nchini Yemen
Jun 12, 2018 09:14Ndege za kivita za Saudi Arabia zimedondosha mabomu katika kituo kimoja cha afya cha kuwatibu watu wenye kipindupindu nchini Yemen ambacho kinasimamiwa na Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF).