-
Wanajeshi zaidi ya 1,000 wa Saudia wameuawa katika vita dhidi ya Yemen
May 29, 2018 09:19Zaidi ya wanajeshi 1,000 wa Saudi Arabia wameuawa katika uvamizi wa nchi hiyo dhidi ya Yemen ulioanza Machi 2015.
-
Mgogoro wa Qatar na nchi za Kiarabu wazidi kutokota, Doha yapiga marufuku bidhaa za Saudia, Imarati, Bahrain na Misri
May 27, 2018 00:13Katika hali inayoonekana ni kuzidi kuwa mkubwa mgogoro wa Qatar na nchi nne za Kiarabu zilizoizingira kila upande nchini hiyo, wizara ya uchumi na biashara ya Qatar jana ilipiga marufuku kuhifadhi, kunua na kuuza bidhaa yoyote iliyotengenezwa Saudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu yaani Imarati, Bahrain na Misri.
-
Ethiopia yamwita nyumbani balozi wake mdogo kutoka Saudia
May 24, 2018 02:55Vyombo vya habari vya nchi za Kiarabu vimetangaza kuwa, baada ya Ethiopia kumwita nyumbani balozi wake kutoka Riyadh, mji mkuu wa Saudi Arabia, imemwita nyumbani pia balozi wake mdogo aliyekuweko mjini Jeddah.
-
Mwakilishi wa Iran UN: Marekani imewapatia kinga Wazayuni na Wasaudi ya kushambulia raia
May 22, 2018 23:55Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema utawala wa Kizayuni na ule wa Aal Saud zinaungwa mkono na Marekani kwa kuwa ni mwanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama katika mashambulio yao dhidi ya raia na kubainisha kuwa Washington imezipatia kinga tawala mbili hizo.
-
Raia karibu 700 wa Ethiopia waliokuwa wamefungwa Saudia warejeshwa kwao
May 21, 2018 03:22Wizara ya Mambo ya Nje ya Ethiopia imesema kuwa, karibu raia 700 wa nchi hiyo waliokuwa wamefungwa nchini Saudi Arabia, wamerejea nyumbani.
-
Saudia yaanza duru mpya ya kuwakamata wale wanaopinga nchi hiyo kuwa na uhusiano na Israel
May 19, 2018 21:52Vyombo vya habari, wanasheria na wanaharakati mbalimbali wameelezea kupitia mitandao ya kijamii juu ya kuanza duru mpya ya kamatakamata ya utawala wa kifalme wa Aal-Saud dhidi ya wapinzani wanaopinga nchi hiyo kuwa na uhusiano na utawala katili wa Kizayuni.
-
Mwanamfalme wa Qatar: Saudia iliyoiuza al-Aqsa kwa adui, haina haki ya kusimamia al-Kaabah
May 19, 2018 09:35Mjukuu wa mwasisi wa taifa la Qatar sambamba na kukosoa vikali mienendo ya Mfalme Salman bin Abdulaziz Al Saud wa Saudi Arabia kwa kuitumikia Marekani na utawala wa Kizayuni, amesema kuwa mtu ambaye ameiuza Masjidul-Aqsa kwa adui wa Uislamu, hafai kuwa msimamizi wa nyumba ya Mwenyezi Mungu ya al-Kaabah.
-
Maroketi ya Yemen yasambaratisha kambi ya jeshi ya Saudia, Najran
May 13, 2018 03:27Vikosi vya Jeshi la Yemen vimevurumisha maroketi katika kambi moja ya kijeshi ya Saudi Arabia katika mkoa wa kusini wa Najran, na kuharibu silaha nyingine kikiwemo kifaru cha kijeshi.
-
Saudia yatumia tena mabomu ya vishada 'yaliyopigwa marufuku' dhidi ya raia wa Yemen
May 12, 2018 22:17Shirika la Habari la Al-Masdar News limeripoti kwamba, Saudia imetumia kwa mara nyingine mabomu ya vishada katika maeneo tofauti ya Yemen dhidi ya raia wa taifa hilo.
-
Kushtadi hitilafu baina ya Imarati na Saudi Arabia huko Yemen; Imarati yakivamia kisiwa cha Socotra
May 04, 2018 23:34Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) umekivamia na kukikalia kwa mabavu kisiwa cha Socotra huko Yemen na kuvifukuza vikosi vyenye mfungamano na Rais mtoro wa nchi hiyo kisiwani humo.