-
Watetezi wa haki za binadamu: Saudia inazusha machafuko na hitilafu Mashariki ya Kati
Apr 02, 2017 11:34Jumuiya na watetezi wa haki za binadamu wamesema kuwa Saudi Arabia ndiyo sababu kuu ya machafuko na ghasia zinazoshuhudiwa kwa sasa katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Chama cha Sinn Féin chataka Uingereza isiiuzie Saudia silaha
Apr 01, 2017 23:50Chama cha Sinn Féin cha Ireland Kaskazini nchini Uingereza kimetoa taarifa kikitaka serikali ya nchi hiyo isitishe mara moja uuzaji silaha kwa utawala wa Saudi Arabia.
-
Kamanda wa jeshi la Saudia apigwa mayai Uingereza
Mar 31, 2017 02:55Ahmed al-Asiri, mshauri wa Wizara ya Ulinzi ya Saudia na msemaji wa muungano vamizi wa Saudia dhidi ya Yemen, ameshambuliwa na waandamanaji wanaopinga hujuma za utawala wa Aal-Saud nchini Yemen na kupigwa mayai mabovu.
-
Zaidi ya mamluki 100 wa Saudia waangamizwa ndani ya siku tatu nchini Yemen
Mar 31, 2017 02:33Wizara ya Ulinzi nchini Yemen imetangaza kuwa, zaidi ya mamluki 100 wa utawala wa Aal Saud wameuawa katika mashambulizi ya makombora na mizinga iliyovurumishwa na jeshi hilo katika kipindi cha siku tatu zilizopita.
-
Maandamano Sana'a kulaani vita vya Saudia dhidi ya Yemen
Mar 26, 2017 10:27Mamilioni ya wananchi wa Yemen wameandamana leo katika mji mkuu Sana'a na maeneo mengine nchini humo katika mwanzo wa mwaka wa tatu tokea Saudia ianzishe vita vyake vya kinyama dhidi ya nchi hiyo ambavyo vimesababisha maelfu ya watu kupoteza maisha na wengine wengi kupoteza makazi yao.
-
Ufaransa inaiuzia Saudia silaha za kuwaulia raia waliodhulumiwa wa Yemen
Mar 21, 2017 11:31Rais wa Ufaransa ametoa kibali cha kuuzia silaha utawala wa Aal Saud na hivyo kuuchochea waziwazi utawala huo kuendelea kuwauwa wananchi wa wasio na ulinzi na waliodhulumika wa Yemen.
-
Familia za wahanga wa Septemba 11, zafungua mashtaka dhidi ya Saudi Arabia
Mar 21, 2017 10:01Familia za wahanga waliopoteza maisha katika mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11 mwaka 2001 nchini Marekani wamefungua mashtaka dhidi ya utawala wa kifalme wa Saudi Arabia.
-
Jeshi la Yemen: Sasa Saudia ijiandae kwa operesheni mpya ndani ya nchi hiyo
Mar 21, 2017 04:18Naibu Msemaji wa Jeshi la Yemen, ameionya Saudi Arabia kwamba, ikiwa itaendelea kushambulia bandari za Yemen, basi jeshi la nchi hiyo na harakati ya wananchi ya Answarullah, zitafanya operesheni ndani ya ardhi ya Saudia.
-
Waziri Mkuu wa Somalia: Saudia, mhusika wa mauaji ya wakimbizi wa Kisomali
Mar 20, 2017 11:38Serikali ya Somalia imesema kuwa utawala wa Saudi Arabia ndio uliohusika na mauaji ya wakimbizi wa nchi hiyo katika maji ya Yemen.
-
Saudia yaitaka UN isimamie bandari ya Yemen baada ya kuua kikatili Wasomali 44
Mar 20, 2017 04:31Muungano vamizi wa kijeshi wa Saudi Arabia nchini Yemen umeutaka Umoja wa Mataifa uchukue udhibiti wa bandari ya Hudaydah baada ya helikopta ya Aal-Saud aina ya Apache kufanya shambulio la kikatili dhidi ya boti ya wakimbizi karibu na Lango Bahari la Bab al-Mandab, pwani ya Yemen na kuua makumi ya raia wa Somalia.