-
Jeshi la Somalia lazima shambulizi la al Shabab dhidi ya Ikulu ya Rais mjini Mogadishu
Dec 11, 2019 03:21Jeshi la Somalia limetangaza kuwa, limewaangamiza wapiganaji 5 wa kundi la kigaidi la al Shabab waliojaribu kuingia na kuhujumu Ikulu ya Rais na hoteli moja iliyoko karibu na eneo hilo mjini Mogadishu.
-
Jubaland: Majeshi ya Ethiopia na Somalia yanataka kumpindua Rais Madobe
Nov 17, 2019 04:16Serikali ya eneo lenye mamlaka ya ndani la Jubaland, Kusini mwa Somalia imedai kuwa wanajeshi wa Ethiopia wanakula njama za kumpindua Rais Ahmed Madobe wa jimbo hilo.
-
OCHA: Mafuriko yameua watu 17 Somalia, 370,000 waachwa bila makazi
Nov 06, 2019 21:44Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu (OCHA) imesema watu wasiopungua 17 wameaga dunia baada ya kusombwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini Somalia.
-
UN yatuma misaada kufuatia maafa ya mafuriko nchini Somalia
Nov 03, 2019 09:12Umoja wa Mataifa umetuma misaada ya dharura nchini Somalia kufuatia mvua kubwa ambazo zimenyesha katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo na kusababisha mafuriko.
-
UN: Nchi za Pembe ya Afrika zinahitaji misaada baada ya mafuriko
Oct 30, 2019 08:12Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mengi ya nchi za Pembe ya Afrika katika miezi michache iliyopita zimesababisha mafuriko na mahitaji ya misaada ya kibinadamu hususan nchini Ethiopia, Sudan Kusini na Somalia.
-
Athari za mvua Somalia, watu 15 wahofiwa kufa maji katika ajali ya boti
Oct 29, 2019 04:25Kwa akali watu 15 wanahofiwa kupoteza maisha katika ajali ya kuzama boti katika mji wa Beledweyn katikati ya Somalia, huku athari za mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika zikiendelea kushuhudiwa.
-
Raia 3 wa Somalia 'watoweka' kufuatia shambulizi la anga la Marekani
Oct 26, 2019 08:27Kwa akali raia watatu wanahofiwa kuuawa katika shambulizi la anga lililofanywa na ndege isiyo na rubani 'drone' ya Marekani katika eneo la Puntland, kaskazini mashariki mwa Somalia.
-
Ripoti: Mabadiliko ya tabianchi yanakwamisha jitihada za kurejesha amani Somalia
Oct 23, 2019 23:19Ripoti mpya ya Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Amani ya Stockholm (SIPRI) inaonyesha kuwa, mabadiliko ya tabianchi yamedumaza jitihada za sasa na za baadaye za kurejesha amani na utulivu nchini Somalia.
-
Wanachama 20 wa kundi la ash-Shabab, wauawa nchini Somalia
Oct 19, 2019 23:05Maafisa wa serikali ya Somalia wametangaza habari ya kuuawa wanachama 20 wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la ash-Shabab katika shambulizi lililolilenga gari yao katikati mwa nchi hiyo.
-
Magaidi 11 wa al-Shabaab wauawa na jeshi la Somalia wakikusanya ushuru
Oct 16, 2019 04:12Askari wa Jeshi la Taifa la Somalia wamefanikiwa kuwaangamiza wanachama 11 wa kundi la kigaidi la al-Shabaab katika operesheni ya jana Jumanne kwenye eneo la Gedo, kusini mwa nchi.