-
Wasudani wapinga mwenendo wa kuanzisha uhusiano na utawala haramu wa Israel
Oct 17, 2022 07:30Katika kikao kinachofanyika mjini Khartoum kuhusu suala la Palestina, makundi ya Kiislamu ya Sudan yametahadharisha kuhusu hatua ya Waarabu ya kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
14 wauawa, kujeruhiwa katika mapigano ya kikabila nchini Sudan
Oct 16, 2022 08:03Kwa akali watu watano wameuawa huku wengine tisa wakijeruhiwa katika mapigano mapya ya kikabila katika eneo la Kordofan Magharibi nchini Sudan.
-
Al-Burhan: Inawezekana kufikia makubaliano kuhusu Bwawa la Renaissance
Oct 16, 2022 03:28Mkuu wa Baraza la Utawala la Sudan ambaye pia ni kamanda wa jeshi la nchi hiyo amesema, kuna uwezekano wa kufikiwa mapatano kuhusu Bwawa na Renaissance.
-
Mafuriko yaliyosababishwa na mvua yaua watu zaidi ya 130 nchini Sudan
Sep 17, 2022 03:03Watu 134 wamepoteza maisha nchini Sudan baada ya kusombwa na maji kufuatia mafuriko makubwa yanayosababishwa na mvua kali inayoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo.
-
Sudan yachapisha rasimu ya katiba mpya
Sep 13, 2022 03:44Serikali ya ya Sudan imechapisha rasimu ya katiba mpya ya nchi hiyo kwa lengo la kuunda mfumo wa kidemokrasia wa mpito ili kukomesha mgogoro uliopo nchini humo.
-
Al-Burhan: Taasisi za kiraia zisiingilie masuala ya jeshi la Sudan
Sep 07, 2022 22:20Mkuu wa baraza tawala la Sudan ameonya kuhusu uingiliaji wowote wa makundi ya kiraia ya nchi hiyo katika taasisi ya kijeshi.
-
Viongozi wa upinzani Sudan wasisitiza kuunga mkono maandamano ya wananchi
Sep 03, 2022 07:03Viongozi wa harakati na makundi ya uhuru na mageuzi nchini Sudan wamesisitiza kuwa, wanaunga mkono maandamano ya amani ya wananchi wa nchi hiyo kwa ajili ya kuuangusha utawala wa kijeshi unaoongozwa na jenerali Abdul-Fattah al-Burhan.
-
Kadhaa wauawa katika mapigano mapya ya kikabila Blue Nile, Sudan
Sep 02, 2022 07:30Kwa akali watu saba wameuawa huku makumi ya wengine wakijeruhiwa katika mapigano mapya ya kikabila yaliyozuka katika jimbo la Blue Nile, kusini mwa Sudan.
-
Sudan yamwita balozi wa Ethiopia kulalamikia madai ya Addis Ababa kuhusu silaha za wapiganaji wa Tigray
Aug 31, 2022 06:57Wizara ya Masshauri ya Kigeni ya Sudan imemwita katika makao makuu ya wizara hiyo balozi wa Ethiopia mjini Kharton na kumkabidhi malalamiko dhidi ya madai ya serikali ya Addis Ababa ya kupita katika anga ya Sudan ndege iliyokuwa imebeba silaha kwa ajili ya kuwapelekea wapiganaji wa jimbo la Tigray.
-
Abdul-Fattah al-Burhan afanya mabadiliko makubwa katika jeshi la Sudan
Aug 26, 2022 05:22Jenerali Abdul-Fattah al-Burhan, kiongozi wa kijeshi nchini Sudan, ametangaza mabadiliko makubwa ya uongozi katika jeshi la nchi hiyo, huku msukosuko wa kisiasa na kiuchumi ukiendelea kushuhudiwa nchini humo.