-
Sudan yalaani vikwazo vipya vya Umoja wa Ulaya dhidi yake
Jul 20, 2025 14:07Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan imeshutumu vikwazo vipya vilivyowekwa na Umoja wa Ulaya dhidi ya watu binafsi na mashirika ya Sudan, na kusisitiza kuwa havina "viwango vya uadilifu vya kisheria."
-
UN yalaani mauaji ya raia yaliyofanywa na pande zote mbili katika vita vya Sudan
Jul 18, 2025 05:28Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, amelaani mauaji ya raia kadhaa yaliyofanywa wiki iliyopita na pande zote mbili husika katika vita vya Sudan, katika mapigano yanayoendelea kwenye eneo la Kordofan.
-
UN: Tuna wasiwasi kutokana na kushtadi mapigano, taharuki Sudan
Jul 16, 2025 12:41Wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wamesema wana wasiwasi mkubwa kutokana na kuongezeka kwa mapigano nchini Sudan, hasa mashambulizi ya karibuni katika Jimbo la Kordofan Kaskazini.
-
Wanaharakati Sudan: RSF imeua watu 300 Kordofan Kaskazini
Jul 15, 2025 04:23Wanaharakati wa Sudan wamesema Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kimeua karibu watu 300 katika wimbi jipya la mashambulizi katika jimbo la Kordofan Kaskazini, magharibi mwa nchi.
-
ICC: Uhalifu wa kivita, jinai dhidi ya binadamu vinaendelea Darfur, Sudan
Jul 11, 2025 14:53Naibu Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC amesema kuna "sababu za kuamini kwamba uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu" unaendelea kufanywa katika eneo la magharibi mwa Sudan la Darfur,
-
IOM: Mamia ya familia za raia wa Sudan watoroka Kordofan kutoka na vita
Jul 10, 2025 21:06Mapigano kati ya jeshi la Sudan na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) yamelazimisha familia 700 kulikimbia Jimbo la Kordofan Kaskazini, huko kusini mwa Sudan, Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) lilisema hayo jana Alkhamisi.
-
Takriban watoto 239 wamefariki dunia magharibi mwa Sudan tangu Januari
Jun 30, 2025 08:00Takriban watoto 239 wameaga dunia magharibi mwa Sudan tangu mwezi Januari mwaka huu kutokana na ukosefu wa chakula na dawa za kutosha. Ripoti hii imetolewa na Mtandao wa Madaktari wa Sudan.
-
RSF yashambulia tena kambi ya wakimbizi na kuua 14 Darfur, Sudan
Jun 05, 2025 06:52Kwa akali watu 14 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika shambulizi la mizinga la Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) katika jimbo la Darfur Kaskazini, magharibi mwa Sudan.
-
UNHCR: Mgogoro mpya Sudan Kusini “umeng’oa” zaidi ya watu 165,000 ndani ya miezi mitatu
Jun 04, 2025 13:13Zaidi ya watu 165,000 wamelazimika kukimbia makazi yao na kukimbilia usalama wao maeneo mengi kutokana na mivutano na migogoro ambayo inazidi kuongezeka nchini Sudan Kusini katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.
-
UN: Wakimbizi milioni 4 wametoroka vita Sudan
Jun 04, 2025 06:08Umoja wa Mataifa umesema zaidi ya watu milioni 4 wamekimbia vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan.