Machafuko na ukosefu wa usalama vinaweza kushtadi huko Sudan Kusini baada ya moja ya mabomba yake makuu ya mafuta linaloelekea katika masoko ya kimataifa kupitia nchi jirani ya Sudan kuathirika mwezi uliopita. Haya ni kwa mujibu wa wataalamu wa masuala ya uchumi. Wamesema kuwa kusitishwa uzalishaji wa mafuta huko Sudan Kusini kunaweza kuchochea pakubwa ghasia na ukosefu wa usalama nchini humo.
Hali ya wasi wasi imetanda nchini Sudan Kusini kufuatia mauaji ya watu 15 yaliyotokea katika eneo la Pibor, mashariki mwa nchi hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan Kusini amesema moja ya changamoto kuu zinazozikabili nchi maskini za ulimwengu wa tatu ni vikwazo vya madola makubwa duniani dhidi yazo.
Kwa akali watu sita wameuawa katika shambulizi linaloamini ni la ulipizaji kisasi katika eneo linalozozaniwa la Abyei, kwenye mpaka wa Sudan na Sudan Kusini.
Umoja wa Mataifa umelaani vikali machafuko ya hivi karibuni katika jimbo la Warrap na katika eneo la Abyei ambayo tangu mwezi uliopita hadi sasa yamesababisha kuuawa makumi ya watu.
Mashirika ya kibindamu ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini yametahadharisha kuhusu ongezeko kubwa la watu wanaorejea na wakimbizi wanaokimbia mzozo na kuelekea kaskazini nchini Sudan.
Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir amesema karibuni hivi atakuwa mwenyeji wa mkutano utakaowaleta pamoja viongozi wa pande mbili zinazopigana nchini Sudan, yaani Jeshi la Taifa la Sudan (SAF) na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF)
Maafisa wa serikali ya Sudan Kusini wamesema mamilioni ya watoto nchini humo wapo katika hatari ya kupoteza maisha kutokana na mgogoro wa njaa unaolikabili taifa hilo changa zaidi barani Afrika.
Watu wasiopungua 13 wameuawa katika mapigano mapya ya kikabila katika nchi ya Sudan Kusini.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha uamuzi wa kuongezea muda wa Operesheni Maalumu ya Kulinda Amani ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) kwa mwaka mmoja, hadi tarehe 15, Machi mwaka 2024.