-
Rais wa Syria asisitiza ulazima wa kupambana na misingi ya kifikra ya ugaidi
Aug 26, 2022 22:52Rais Bashar al Assad wa Syria amesisitiza ulazima wa kupambana na misingi ya kifikra ya ugaidi na akaeleza kwamba, kupambana na ugaidi hakutawezekana kwa kutumia nguvu za kijeshi pekee, kwa sababu idiolojia ya mitazamo ya kufurutu ada haitambui mipaka bali inajipanua na kuenea kwa kasi kutoka nchi moja hadi nyingine.
-
Erdoğan: Uturuki haipiganii kumwondoa Bashar al Assad katika mfumo wa kisiasa wa Syria
Aug 20, 2022 22:13Katika mwendelezo wa kauli zinazogongana ambazo zinatolewa na viongozi wa Uturuki kuhusu Syria, rais wa nchi hiyo Recep Tayyip Erdoğan amedai kuwa Uturuki haipiganii kumwondoa katika muundo wa kisiasa Rais Bashar al Assad wa nchi hiyo.
-
Marekani inaiba 80% ya mafuta yanayozalishwa Syria kila siku
Aug 16, 2022 03:09Marekani inapora asilimia 80 ya mafuta yanayozalishwa kwa siku nchini Syria.
-
Magaidi 50 wa Daesh wahamishiwa Iraq kutoka nchini Syria
Aug 13, 2022 22:01Kitengo cha upashaji habari cha jeshi la Iraq kimetoa ripoti rasmi na kusema kuwa karibu wanachama 50 wa genge la kigaidi na ukufurishaji la Dashe (ISIS) wamehamishiwa mkoani Nainawa (Nineveh) Iraq kutoka katika kambi ya al Hawl ya nchini Syria.
-
Russia: Kuondoka majeshi ya Marekani Syria kutarahisisha na kuharakisha kuangamizwa magaidi
Aug 10, 2022 03:14Mwakilishi wa kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa amesema, kuondoka majeshi ya Marekani Syria kutarahisisha na kusahilisha kwa haraka zaidi kuangamizwa magaidi katika nchi hiyo.
-
Syria: Tumejiweka tayari kukabiliana na shambulio lolote litakalofanywa na Uturuki
Jul 27, 2022 03:33Wizara ya ulinzi ya Syria imetangaza kuwa jeshi la nchi hiyo limejiweka tayari kikamilifu kukabiliana na shambulio lolote linaloweza kufanywa na Uturuki na makundi inayoyaunga mkono.
-
Kwa mara nyingine China yataka Syria iondolewe vikwazo
Jul 25, 2022 21:57Naibu mwakilishi wa kudumu wa China katika Umoja wa Mataifa amesisitiza kwamba kuna wajibu wa kuondolewa haraka vikwazo ilivyowekewa Syria kwani vikwazo hivyo vinakwamisha juhudi za kupeleka misaada ya kibinadamu nchini humo.
-
Jeshi la Syria latungua makombora ya Israel viungani mwa Damascus
Jul 22, 2022 02:41Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Syria kimetangaza kutungua makombora yaliyokuwa yamevurumishwa na utawala haramu wa Israel nje ya mji mkuu Damascus.
-
Mafanikio ya mkutano wa Tehran katika matamshi ya Erdoğan
Jul 21, 2022 22:02Kama ilivyotazamiwa, Mkutano wa 7 wa "Dhamana ya Mchakato wa Astana" uliofanyika majuzi mjini Tehran umekuwa na mafanikio makubwa kuhusu masuala yanayohusiana na serikali halali ya Rais Bashar al-Assad wa Syria na watu wa nchi hiyo.
-
Rais wa Iran apongeza mapambano ya watu wa Syria
Jul 21, 2022 03:04Rais Ebrahim Raeisi wa Iran amesema ana yakini kuwa Syria ina mustakakbali mwema huku akiwapongeza wananchi wa Syria kwa mapambano na muqawama katika kipindi cha miaka 11 ya vita dhidi ya nchi hiyo ambavyo vinaungwa mkono na madola ya kigeni.