-
Iran na Qatar zasisitiza kuzuiwa mashambulio ya Israel dhidi ya miundomsingi ya Syria
Dec 12, 2024 07:38Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Qatar wamesisitiza juu ya ulazima wa kufanyika juhudi na kuchukuliwa hatua za dhati ili kusimamisha mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya miundomsingi ya Syria na kukalia kwa mabavu maeneo zaidi ya nchi hiyo na utawala huo ghasibu.
-
Uturuki yatangaza kufikiwa 'suluhu ya kihistoria' kati ya Ethiopia na Somalia
Dec 12, 2024 07:03Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amempongeza Rais wa Somalia na Waziri Mkuu wa Ethiopia kwa kufikia "suluhu ya kihistoria na kujitolea kwa hali ya juu" katika mazungumzo ya amani baina ya nchi hizo mbili yaliyofanyika mjini Ankara, lengo likiwa ni kumaliza mgogoro wa eneo lililojitenga la Somaliland.
-
Vyombo vya Magharibi vyaakisi kwa wingi miongozo ya Kiongozi Muadhamu
Dec 12, 2024 03:01Mashirika ya habari ya nchi za Magharibi yameakisi kwa wingi hotuba na miongozo muhimu ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei aliyotoa jana Jumatano akisisitiza kuwa Marekani na utawala wa Kizayuni ni wahusika wakuu wa matukio ya Syria.
-
Marekani yakiri kuwa na mkono katika matukio ya sasa nchini Syria
Dec 11, 2024 04:02Kufuatia matukio ya sasa, ya haraka na ya ghafla ya kijeshi nchini Syria na kutekwa Damascus na makundi yenye silaha na hatimaye kuondoka madarakani Rais wa Syria Bashar al-Assad, Marekani imekiri kwamba imekuwa na nafasi katika matukio hayo.
-
UN yatoa indhari ya kuzidi kuharibika hali usalama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Dec 10, 2024 07:58Mwakilishi Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) amesema, kuna mvutano wa kisiasa nchini humo kufuatia miito ya kuifanyia mabadiliko Katiba sambamba na kuzidi kuvurugika hali ya usalama katika mikoa ya Kivu Kaskazini na Ituri kunakohusisha harakati za makundi ya ADF, M23, CODECO na Zaire.
-
Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran kuhusu matukio ya Syria
Dec 09, 2024 00:15Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran imesisitiza kuwa, kuainishwa hatima na kufanya maamuzi kuhusu mustakbali wa Syria ni jukumu la pekee la wananchi wa nchi hiyo bila ya uingiliaji haribifu wala kulazimishwa na mataifa ya kigeni.
-
Reuters: Utawala wa Bashar al-Assad umeanguka, Waziri Mkuu wa Syria: Tuko tayari kukabidhi madaraka
Dec 08, 2024 01:54Shirika la habari la Reuters limenukuu vyanzo vya jeshi la Syria vikisema kuwa maafisa wa ngazi za juu wa jeshi wametangaza kuanguka utawala wa Rais Bashar Assad kwa makamanda wa kijeshi.
-
Waziri wa Ulinzi: Jeshi la Syria bado liko Hama
Dec 06, 2024 08:51Waziri wa Ulinzi wa Syria, Luteni Jenerali Ali Mahmoud Abbas, amesema kuwa hali ya mambo katika mji wa Hama imedhibitiwa na kwamba kusonga mbele kwa awali magaidi wa Kitakfiri katika mji huo kulitokana na mbinu za muda za vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo
-
Sisitizo la Araghchi juu ya haja ya kukabiliana na makundi ya kigaidi nchini Syria
Dec 05, 2024 04:46Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya ulazima wa kuweko uratibu wa nchi za kieneo na jibu la haraka la jamii ya kimataifa katika kukabiliana na makundi ya kigaidi nchini Syria.
-
Iravani: Iran itaendelea kuwa imara katika kuiunga mkono Syria
Dec 04, 2024 09:35Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amezungumzia machafuko ya karibuni ya magaidi huko Syria na kusisitiza kuwa Tehran itaendelea kuiunga mkono Damascus katika kukabiliana na makundi hayo ya kigaidi.