-
Rais wa Sudan awa kiongozi wa mwanzo wa Arab League kuitembelea Syria miaka 8 tangu vilipoanza vita
Dec 17, 2018 00:36Rais Omar al-Bashir wa Sudan amefanya safari nchini Syria na kuwa kiongozi wa kwanza wa nchi mwanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) kuitembelea nchi hiyo tangu ulipoanza mgogoro wa ndani miaka minane iliyopita.
-
Ndege za kivita za Saudia zaishambulia Hudaydah licha ya mapatano
Dec 15, 2018 04:05Ndege za kivita za Saudi Arabia zimeshambulia kwa mabomu mji wa al-Hudaydah, siku moja baada ya kufikiwa mapatano baina ya pande mbili nchini Yemen, kufuatia mazungumzo yaliyohusu mji huo wa bandari wa magharibi mwa nchi yanayosimamiwa na Umoja wa Mataifa.
-
Wasiwasi wa kuongezeka misaada ya Magharibi kwa magaidi wa Syria
Dec 15, 2018 02:55Tangu mwaka 2011 yalipoanzishwa machafuko nchini Syria hadi hivi sasa, nchi za Magharibi hasa Marekani, Uingereza na Ufaransa pamoja na vibaraka wao baadhi ya nchi za Kiarabu zimekuwa zikiyaunga mkono kwa hali na mali magenge ya kigaidi kwa tamaa ya kuipindua serikali iliyoko madarakani kihalali nchini Syria.
-
Syria kurejeshewa uanachama wa Arab League baada ya kupita miaka saba?
Dec 14, 2018 23:11Bunge la Jumuiya ya Nchi za Kiarabu limeitaka Arab League iirejeshe Syria kuwa mwanachama wake, miaka saba baada ya kuvuliwa uanachama huo.
-
Raia 200 wakombolewa kutoka mikononi mwa magaidi, Deir ez-Zor, Syria
Dec 10, 2018 12:38Baada ya mapambano makali na genge la kigaidi la Daesh katika mji wa Hajin wa mkoa wa Deir ez-Zor wa mashariki mwa Syria, hatimaye wanamgambo wa Kikurdi wanaojulikana kwa jina la Askari wa Demokrasia wa Syria wamefanikiwa kuwakomboa raia 200 waliokuwa chini ya udhibiti wa magaidi hao wakufurishaji.
-
Njama mpya za Marekani za kuunda jeshi la kieneo nchini Syria
Dec 09, 2018 23:24Mkuu wa Jeshi la Marekani amesema kuwa nchi hiyo ina nia ya kuanzisha na kulipa mafunzo jeshi la watu 40 elfu mashariki mwa Syria kwa madai ya kuleta utulivu katika eneo hilo.
-
Marekani yaendeleza umwagaji damu Syria, yaua watu 8 wa familia moja
Dec 07, 2018 20:55Muungano wa eti kupambana na magaidi wa Daesh unaoongozwa na Marekani umeendelea kufanya mashambulizi yake ya anga katika mkoa wa mashariki wa Deir ez-Zor nchini Syria na kuua raia wengi.
-
UN: Magaidi wa Daesh wanawachinja raia wa Syria, Deir ez-Zor
Dec 05, 2018 23:15Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ametoa indhari juu ya kuendelea kuwa mbaya hali ya kibinadamu nchini Syria, na kushtadi mauaji ya raia yanayofanywa na wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) mashariki mwa nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Magaidi Syria wapokea 'drones' 100 za kufanya hujuma za kemikali Idlib
Dec 04, 2018 11:13Kundi la kigaidi la Jabhatu Nusra la Syria limepokea ndege zisizo na rubani zipatazo 100 litakazozitumia kufanya mashambulizi ya kemikali za sumu katika mkoa wa Idlib, kaskazini magharibi mwa nchi.
-
UN yaitaka Israel iondoke kwenye Miinuko ya Golan ya Syria
Dec 01, 2018 04:35Kwa mara nyingine tena Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepasisha kwa wingi wa kura azimio la kuutaka utawala ghasibu wa Israel kuondoka katika eneo la Miinuko ya Golan la Syria ambalo umelikalia kwa mabavu kwa karibu nusu karne sasa.