-
Kiongozi Muadhamu: Siku ya kusali sala ya jamaa Quds itafika karibuni hivi
Mar 01, 2018 12:10Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, leo Alkhamisi ameonana na kundi la maulamaa wa Syria na kusisitizia wajibu wa kushikamana vilivyo na mambo yanayowaunganisha Waislamu wote. Amesema: Ni matumaini yetu sote tutaiona siku ambayo mtasali sala la jamaa mjini Quds na siku hiyo haiko mbali tena bali itafika karibuni hivi, ni sawa tu kama watu kama sisi tutakuwa bado tupo au hatupo tena.
-
Mogherini ataka kuandaliwa mazingira ya kusimamisha vita kote nchini Syria
Feb 28, 2018 12:58Mkuu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya ameziomba Russia, Iran na Uturuki ziandae mazingira ya kusimamisha mapigano huko Syria.
-
Hujuma za anga za Marekani zaendelea kuteketeza roho za Wasyria
Feb 28, 2018 04:32Makumi ya raia wameuawa kufuatia mashambulizi ya anga ya Marekani mashariki mwa mkoa wa Dayr al-Zawr nchini Syria.
-
Silaha za Israel zapatikana katika ngome za ISIS (Daesh) Syria
Feb 27, 2018 22:02Vyombo vya habari nchini Syria vimerusha kanda ya video inayoonyesha silaha zilizotengenezewa Israel, katika maeneo yaliyokombolewa hivi karibuni kutoka kwenye makucha ya kundi la kigaidi la Daesh (ISIS), mkoani Dayr al-Zawr.
-
Silaha za Marekani ilizowapa magaidi Syria zapigwa mnada katika Intaneti! Russia yaonya kutumika silaha za kemikali
Feb 26, 2018 04:00Televisheni ya CNN ya Marekani imefichua kuwa, silaha za nchi hiyo walizopewa magaidi nchini Syria zinapigwa mnada kwenye Intaneti. Hayo yametangazwa huku Russia ikitahadharisha kuwa magaidi wamepanga kufanya mashambulizi ya kemikali na baadaye kuisingizia serikali ya Syria.
-
Baraza la Usalama la UN lapasisha azimio la kusitisha vita kwa siku 30 Syria
Feb 24, 2018 23:54Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio la kusitishwa vita kwa siku 30 nchini Syria na kuruhusu upelekaji wa misaada ya kibinadamu katika maeneo yanayozingirwa.
-
Rais Putin awapongeza wanajeshi wa Russia walioko Syria
Feb 24, 2018 10:55Rais Vladimir Putin wa Russia amewapongeza na kuwashukuru wanajeshi wa nchi yake walioko nchini Syria.
-
Araqchi: Uwepo wa Iran nchini Syria ni kwa ajili ya kupambana na ugaidi
Feb 22, 2018 11:06Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, uwepo wa kiushauri wa Iran huko Iraq na Syria na kupambana na ugaidi umeyakwaza makundi ya kigaidi na kuyafanya yashindwe kuwa na udhibiti katika Mashariki ya Kati ikiwemo Lebanon.
-
Syria yaitaka UN kuchukua hatua dhidi ya waungaji mkono ugaidi
Feb 22, 2018 00:59Serikali ya Syria imeuandikia barua Umoja wa Mataifa ikizungumzia ongezeko la mauaji ya kigaidi yanayofanywa dhidi ya raia wa Damascus na vitongoji vyake na kuutaka umoja huo kuchukua hatua dhidi ya nchi zinazoyasaidia na kuyafadhili makundi ya kigaidi.
-
Kufichuliwa uungaji mkono mpya wa utawala wa Kizayuni kwa makundi ya kigaidi nchini Syria
Feb 22, 2018 00:56Katika taarifa yake gazeti la utawala haramu wa Israel la Haaretz limekiri kwamba Tel Aviv inajishughulisha zaidi na kuwapatia silaha magaidi nchini Syria.