-
Algeria yaikosoa Ufaransa kwa kuingilia wimbo wake wa taifa
Jun 24, 2023 02:36Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria ameijia juu Ufaransa kwa kujiingiza kwenye mjadala kuhusu wimbo wa taifa wa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Cameroon: Hatutamruhusu balozi wa Ufaransa kuja nchini kupigia debe ushoga
Jun 22, 2023 07:06Serikali ya Cameroon imesema haitamruhusu kuingia nchini humo balozi wa Ufaransa wa kutetea na kushajiisha vitendo vya ushoga, usagaji na watu kubadili jinsia zao (LGBT).
-
Takwa la Rais wa Ufaransa kwa Ulaya la kujiepusha na utegemezi wa kijeshi kwa Marekani
Jun 20, 2023 12:03Jumatatu ya jana tarehe 19 Juni, Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa alizitaka nchi za Ulaya kutafuta uhuru zaidi katika ulinzi wa anga zao na kuacha kuwa tegemezi kupita kiasi kwa Marekani.
-
Sisitizo la Rais wa Algeria la kuiunga mkono Russia licha ya mashinikizo ya Magharibi
Jun 18, 2023 02:47Rais Abdelmadjid Tebboune wa Algeria siku ya Alkhamisi alisema baada ya kuonana na rais mwenzake wa Russia mjini Moscow kwamba, Algiers iko chini ya mashinikizo makubwa ya madola ya Magharibi yanayoitaka isishirikiane na Moscow kivyovyote vile.
-
Mwenendo unaoongezeka wa vitisho dhidi ya Waislamu nchini Ufaransa
Jun 17, 2023 07:58Katika miaka ya karibuni, wanasiasa wa Ufaransa wamekuwa wakiwawekea vikwazo Waislamu na kuchochea chuki dhidi ya Uislamu katika nchi hiyo.
-
Katika uamuzi wa aina yake.. Rais wa zamani wa Ufaransa ahukumiwa kifungo miaka 3 jela katika kesi ya ufisadi
May 17, 2023 11:09Mahakama ya Rufaa ya Paris leo, Jumatano, imemhukumu Rais wa zamani wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy kifungo cha miaka 3 jela, ambapo anawekwa chini ya uangalizi kwa kufungwa bangili ya kielektroniki. Ni baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika na ufisadi na kutumia vibaya madaraka, hatua ambayo haijawahi kushuhudiwa dhidi ya rais wa zamani wa Ufaransa.
-
Ombi la Ufaransa na Marekani kwa China kuitaka iwe msuluhishi katika vita vya Ukraine
Apr 07, 2023 08:19Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa siku ya Jumatano aliwasili Beijing kwa ziara ya siku tatu nchini China. Ziara hiyo ni ya kwanza kufanywa na Macron nchini China tangu mwaka 2019. Rais huyo wa Ufaransa jana alifanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Xi Jinping.
-
Burkina Faso yawafukuza wanahabari wa magazeti ya Ufaransa
Apr 03, 2023 03:22Serikali ya kijeshi ya Burkina Faso imewatimua nchini humo maripota wa magazeti ya Ufaransa ya 'Le Monde' na 'Libération' huo ukiwa ni muendelezo wa hatua za nchi hiyo Afrika Magharibi za kukabiliana na vyombo vya habari vya nchi hiyo ya Ulaya.
-
Burkina Faso yaifungia 'France 24' baada ya mahojiano na al-Qaeda
Mar 28, 2023 02:20Serikali ya kijeshi ya Burkina Faso imesimamisha matangazo ya kanali ya televisheni ya Ufaransa ya France 24, baada ya chombo hicho kurusha hewani mahojiano kiliyoyafanya na kiongozi wa kundi la kigaidi la al-Qaeda tawi la Kaskazini mwa Afrika AQIM.
-
Aliachwa akihangaika na kifo peke yake; Hasira zatanda Ufaransa baada ya kifo cha mwanafunzi mwenye asili ya Kiarabu
Mar 25, 2023 02:20Mitandao ya kijamii nchini Ufaransa imeshuhudia wimbi kubwa la hasira na ghadhabu baada ya kifo cha mwanafunzi mwenye asili ya Kiarabu ambaye alipatwa na mshtuko wa moyo, huku kukiwa na shutuma kwamba uongozi wa shule ulimwacha akikabilina na kifo peke yake bila ya kumpa huduma ya dharura.