-
Erdogan: Dunia ipige vita uadui dhidi ya Uislamu sawa ilivyo katika suala la kupiga vita Uyahudi
Nov 02, 2020 23:15Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki ameitaka dunia ijifunze na kupata somo na ibra kutokana na uzembe wa jamii ya kimataifa iliyoacha kuzuia mauaji ya kimbari ya Waislamu wa Bosnia Herzegovina na kusisitiza kuwa, dunia inapaswa kupiga marufuku na kupambana na chuki na uhasama dhidi ya Uislamu kama ilivyopambana na chuki dhidi ya Uyahudi baada ya Holocaust (yanayodaiwa kuwa mauaji ya Mayahudi wakati wa Vita vya Pili vya Dunia).
-
Rais wa Indonesia akosoa undumakuwili wa Wamagharibi kuhusu uhuru wa kujieleza
Nov 01, 2020 08:19Rais Joko Widodo wa Indonesia amekosoa undumakuwili wa nchi za Magharibi kuhusu uhuru wa maoni na kujieleza na kusema: "Uhuru wa maoni ambao unavunjia heshima matukufu ya kidini haukubaliki."
-
Kukosolewa mwenendo wa sera za chuki dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa
Nov 01, 2020 07:49Kushadidi utendaji ulio dhidi ya Uislamu barani Ulaya hususan nchini Ufaransa katika majuma ya hivi karibuni siyo tu kwamba, kumewakasirisha Waislamu ulimwenguni kote, bali hata viongozi na wanasiasa wa nchi hiyo wameonyesha radiamali zao kwa hatua hiyo.
-
Dunia yaendelea kulaani matamshi ya Rais wa Ufaransa ya kumvunjia heshima Mtume (saw)
Nov 01, 2020 04:40Wimbi kali la kulaani matamshi yaliyotolewa na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa akitetea matusi na kuvunjiwa heshima Mtume Muhammad (saw) nchini humo limeendelea kushuhudiwa katika pembe mbalimbali za dunia.
-
Rais wa zamani wa Ufaransa: Si sahihi kuwahusisha magaidi na Uislamu
Oct 31, 2020 04:08Rais wa zamani wa Ufaransa, François Hollande amemuonya rais wa hivi sasa nchi hiyo Emmanuel Macron na kusema kuwa hapaswi kuwahusisha magaidi na dini ya Uislamu.
-
Wafaransa walitumia mifupa ya wapigania uhuru wa Algeria kutengenezea sabuni
Oct 31, 2020 00:30Mshauri wa masuala ya historia wa Rais wa Algeria amefichua jinai ambazo Ufaransa ilitenda nchini humo katika enzi za ukoloni.
-
Macron aendeleza vitendo vya kuuhujumu Uislamu; Trump aparamia mawimbi
Oct 30, 2020 23:08Kushtadi vitendo vya chuki na hujuma dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa vinavyokwenda sambamba na uungaji mkono wa Rais wa nchi hiyo Emmanuel Macron kwa kisingizio kutetea uhuru wa kusema na kujieleza kumekabiliwa na radiamali mbalimbali na kuifanya nchi hiyo kubwa ya Ulaya ikabiiwe na wimbi kubwa la hasira.
-
Jumuiya Maulamaa wa Palestina: Nchi za Kiislamu zivunje uhusiano wa kidiplomasia na Ufaransa
Oct 30, 2020 13:16Jumuiya ya Maulamaa na Wanatablighi wa Palestina imelaani matamshi ya kifidhuli aliyotoa rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ya kuunga mkono kitendo cha jarida la nchi hiyo la Charlie Hebdo cha kumvunjia heshima Bwana Mtume Muhammad SAW na kuzitolea mwito nchi za Kiislamu wa kuvunja uhusiano wa kidiplomasia na Ufaransa.
-
Waziri Mkuu wa Canada apingana na Macron, asema Uislamu hauna mfungamano na ugaidi
Oct 30, 2020 05:24Waziri Mkuu wa Canada, Justin Trudeau amesema kuwa gaidi aliyetekeleza hujuma ya kigaidi katika mji wa Nice nchini Ufaransa hawakilishi dini ya Uislamu wala Waislamu, na kwamba watu wote wanapasa kukiri ukweli huo.
-
Waislamu wa Ufaransa walaani shambulio la kigaidi lililotokea nchini humo
Oct 29, 2020 23:01Baraza la Waislamu wa Ufaransa limelaani shambulio la kigaidi lililotokea nchini humo.