-
Iran yaangamiza magaidi wanne wa ISIS na kunasa silaha na bendera
Jun 12, 2017 21:56Maafisa wa usalama kusini mwa Iran wamefanikiwa kuwaangamzia magaidi wanne wa kundi la kigaidi la ISIS au Daesh sambamba na kunasa silaha walizokuwa nazo pamoja na bendera ya kundi hilo la kigaidi.
-
Qatar: Tuliwakaribisha Taliban mjini Doha kwa matakwa ya Marekani
Jun 12, 2017 03:21Afisa wa ngazi za juu wa serikali ya Qatar amesema kuwa, nchi hiyo ililialika kundi la kigaidi la Taliban mjini Doha kutokana na takwa la Marekani ambayo leo, ikiwa pamoja na nchi kadhaa za Kiarabu, inaituhuma Qatar kuwa inaunga mkono makundi yenye misimamo mikali.
-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu; kushindwa mfumo wa Ubeberu kuiteteresha irada ya taifa la Iran
Jun 09, 2017 11:16Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema kuhusiana na mashambulio ya kigaidi ya Tehran kuwa taifa la Iran linaendelea kusonga mbele na kwamba harakati za aina hiyo haziwezi kuathiri na kuteteresha irada na azma ya wananchi.
-
Wizara ya Mambo ya Ndani: Mashambulio ya kigaidi Tehran yamehatimishwa, watu 12 wameuawa
Jun 07, 2017 11:13Wizara ya Mambo ya Ndani ya Jamhuri ya Kiislamu ya iran imetangaza kuwa, mashambulio mawili ya kigaidi yaliyotokea leo mjini Tehran yamehatimishwa na kwamba, kila kitu kiko chini ya udhibiti wa vikosi vya usalama.
-
Rais wa Sudan: Ugaidi hauna mafungamano yoyote na Uislamu
Jun 04, 2017 02:53Rais Omar Hassan al-Bashir wa Sudan amesema mashambulizi ya kigaidi ya hivi karibuni katika nchi jirani ya Misri sawa na hujuma nyingine za kigaidi katika sehemu mbali mbali duniani hazina uhusiano wala mafungamano yoyote na dini ya Kiislamu.
-
Kuzidi kuwa mbaya hali ya kibinadamu nchini Chad
Jun 02, 2017 03:08Hali ya kibinadamu nchini Chad na hasa magharibi mwa nchi hiyo katika bonde la Ziwa Chad imeripotiwa kuwa mbaya huku hofu ya kuongezeka idadi ya wahajiri na kumiminika wimbi jipya la wakimbizi katika eneo hilo ikitishia kuifanya hali hiyo iwe mbaya zaidi.
-
Hizbullah: Inashangaza kuona waungaji mkono wa ugaidi wakiuhusisha muqawama na ugaidi
May 29, 2017 09:22Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya nchini Lebanon katika eneo la Beqaa amesema kuwa, anashangazwa na Marekani kuutuhumu muqawama na ugaidi katika hali ambayo ni nchi hiyo ndiyo inayouunga mkono ugaidi wa utawala haramu wa Israel.
-
Kenya kutumia jeshi kutegua mabomu ya barabarani
May 26, 2017 03:24Kenya imetuma wanajeshi katika eneo la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo kwenda kutegua mabomu yaliyotegwa barabarani baada ya watu 20 wakiwemo maafisa 11 kuuawa katika miripuko ya barabarani kwenye eneo hilo.
-
Iran iko tayari kushirikiana na Sierra Leone katika kupambana na ugaidi
May 25, 2017 03:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameashiria mashambulio ya kigaidi katika baadhi ya nchi za Ulaya na Afrika na kutangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kushirikiana na Sierra Leone katika kupambana na ugaidi na misimamo ya kufurutu mpaka.
-
Madai ya waungaji mkono wa magaidi ya kupambana na vyanzo vya kifedha vya magaidi
May 22, 2017 04:35Katika hali ambayo Marekani na baadhi ya nchi za Kiarabu, wanachama wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi ndivyo vyanzo vikuu vya kifedha vya makundi ya kigaidi, jana Jumapili, nchi wanachama wa baraza hilo na Marekani zilikutana mjini Riyadh, Saudi Arabia na kutiliana saini hati ya maelewano kuhusiana na kuanzisha kituo maalumu cha kupambana na waungaji mkono wa kifedha wa makundi ya kigaidi.