-
Watu 16 wauawa katika ghasia za kisiasa Uganda, baada ya Bobi Wine kukamatwa
Nov 19, 2020 11:33Jeshi la Polisi la Uganda limetangaza habari ya kuuawa watu wasiopungua 16 katika maandamano ya fujo yanayoshuhudiwa katika mji mkuu Kampala tokea jana, baada ya kutiwa mbaroni kiongozi wa chama cha upinzani cha National Unity Platform (NUP) ambaye pia na mgombea urais nchini humo, Robert Kyagulanyi, maarufu kwa jina la Bobi Wine.
-
Mkuu wa Tume ya Uchaguzi nchini Uganda aonana na wagombea kutuliza mambo + SAUTI
Nov 16, 2020 12:08Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Uganda amekutana na wagombea urais wa uchaguzi unaotarajiwa kufanyika tarehe 14 Januari 2021 nchini humo, ili kutatua migogoro iliyojitokeza wakati huu wa kampeni za uchaguzi. Maelezo zaidi na mwandishi wetu wa Kampala, Kigozi, Ismail.
-
Wizara ya Afya ya Uganda imeweka kanuni mpya za kudhibiti ugonjwa wa Covid-19 unaoitaabisha dunia nzima hivi sasa + SAUTI
Nov 14, 2020 13:48Wizara ya Afya ya Uganda imeweka kanuni mpya za kudhibiti ugonjwa wa Covid-19 baada ya kukabiliwa na changamoto kali za kuukabili ugonjwa huo unaoitaabisha dunia nzima hivi sasa.
-
Uganda yatangaza tarehe ya uchaguzi mkuu, kampeni kuanza Jumatatu
Nov 05, 2020 08:20Tume ya Uchaguzi Uganda (EC) imetangaza tarehe 14 Januari mwaka ujao 2021 kuwa siku ya kufanyika uchaguzi mkuu ukiwemo wa urais.
-
Mpinzani wa Rais Museven, Bobi Wine akamatwa baada ya kupasishwa kugombea urais
Nov 03, 2020 07:18Kiongozi wa Jukwaa la Umoja wa Kitaifa anayebeba bendera ya chama hicho katika uchaguzi ujao wa rais nchini Uganda, Robert Kyagulanyi maarufu kwa jina la Bobi Wine amekamatwa muda mfupi baada ya kupasishwa kugombea kiti hicho.
-
Licha ya changamoto za corona kwa maisha ya watu, sekta ya kilimo imekuwa na ustawi nchini Uganda + SAUTI
Oct 31, 2020 04:58Sekta ya kilimo imekuwa na ustawi nchini Uganda licha ya hali ngumu inayowakabili wananchi kutokana na janga la Covid-19
-
Polisi ya Uganda yasema imemkamata Bobi Wine kwa kuvaa magwanda ya kijeshi
Oct 15, 2020 04:00Vyombo vya usalama nchini Uganda vimesema lengo la kuvamia makao makuu ya chama cha upinzani cha NUP na kumtia mbaroni Bobi Wine, kinara wa chama hicho anayetazamiwa kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka ujao, ni kukusanya magwanda ya kijeshi yanayovaliwa na wafuasi wa chama hicho.
-
Rais wa Uganda atetea uamuzi wa serikali yake kusaidia ujenzi wa barabara ya kuunganisha nchi hiyo na majirani zake + SAUTI
Oct 12, 2020 12:25Rais Yoweri Museveni wa Uganda Atetea uamuzi wa serikali yake kusaidia ujenzi wa barabara kubwa ya lami ya kuunganisha nchi hiyo na majirani zake wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Sudan Kusini, licha ya Uganda yenyewe kukabiliwa na hali ngumu kiuchumi hivi sasa.
-
Sekta ya usafiri Uganda yalalamikia kubanwa mno wakati wa corona
Oct 02, 2020 15:07Serikali ya Uganda imezidi kupunguza masharti yanayohusiana na ugonjwa wa COVID-19 lakini pamoja na hayo, sekta ya usafiri imekumbwa na changamoto nyingi. Mwandishi wetu wa Kampala, Kigozi Ismail, na maelezo zaidi.
-
EACJ yatupilia mbali faili la ukomo wa urais nchini Uganda
Sep 30, 2020 10:11Mahakama ya Uadilifu ya Afrika Mashariki (EACJ) imetupilia mbali faili lililowasilishwa kwake la kupinga uamuzi wa Mahakama ya Juu ya Uganda, wa kuidhinisha mabadiliko ya katiba yalioondoa ukomo wa umri wa kugombea urais katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.