-
Uganda yakumbwa tena na homa ya Marburg
Oct 20, 2017 13:18Uganda imethibitisha kufariki dunia mtu mmoja kwa homa inayoenezwa na kirusi cha Marburg, homa ambayo huambatana na kuvuja damu sawa kabisa na homa ya Ebola. Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya wa nchi hiyo.
-
Ghasia zashtadi Uganda, Besigye na Wabunge wa upinzani wakamatwa
Oct 20, 2017 04:00Mtu mmoja ameuawa huku wengine sita wakiachwa na majeraha ya risasi na kulazwa hospitalini katika wilaya ya Rukungiri, kufuatia ghasia zilizotokana na maandamano ya kupinga mpango wa kuondoa kikomo cha umri wa kugombea urais nchini Uganda.
-
Uganda yapiga marufuku maandamano ya kupinga kuondolewa kipengee cha umri katika kugombea urais
Oct 18, 2017 11:50Jeshi la polisi nchini Uganda leo (Jumatano) limepiga marufuku kile lilichokiita ni maandamano haramu ya kupinga mpango wa kuondoa kipengee ya umri katika kugombea urais. Juhudi za kuondoa kipengee hicho zina nia ya kumfungulia njia Rais Yoweri Museveni kuendelea kubakia madarakani bila ya kufungwa na kipengee hicho.
-
Kugeuka bunge la Uganda uwanja wa kurushiana makonde
Sep 28, 2017 23:04Mpango wa kuondolewa ukomo wa umri wa rais kwa ajili ya kumuwezesha Rais Yoweri Museven wa Uganda kugombea tena katika uchaguzi wa rais ujao, umepelekea bunge la nchi hiyo kukumbwa na hali ya mchafukoge.
-
Wabunge wa Uganda watwangana tena, matangazo mubashara yafutwa
Sep 27, 2017 10:51Kwa siku ya pili mfululizo, Wabunge wa Uganda wamerushiana makonde Bungeni wakati wa kujadiliwa muswada wa sheria inayotaka kuondoa kikomo cha umri wa kugombea urais nchini humo.
-
Wabunge watwangana makonde Uganda kabla ya kujadili mswada wa kurefusha utawala wa Museveni
Sep 26, 2017 12:35Vurumai za kupigana makonde na kurushiana viti baina ya wabunge zimezuka ndani ya bunge nchini Uganda leo kabla ya bunge hilo kujadili mswada ambao endapo utapitishwa utamwezesha Rais Yoweri Museveni kuwania tena urais kwa kipindi kingine.
-
Mabomu ya kutoa machozi yarindima Uganda huku bunge likijadili mpango wa kurefusha utawala wa Museveni
Sep 21, 2017 11:14Polisi wa Uganda wametumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya watu waliokusanyika kwa lengo la kuandamana kuelekea bungeni kupinga rasimu ya mswada unaolenga kurefusha muda wa kutawala Rais wa nchi hiyo Yoweri Kaguta Museveni. Rasimu hiyo ilitazamiwa kuwasilishwa mbele ya bunge baadaye leo.
-
Wabunge wa upinzani Uganda wadai kutishiwa maisha
Sep 20, 2017 23:18Wabunge wa vyama vya upinzani nchini Uganda wamesema serikali inawatishia maisha masaa machache kabla ya bunge la nchi hiyo kujadili muswada wa kuondoa kikomo cha umri wa kugombea urais nchini humo.
-
Museveni: Kikomo cha umri wa kuwania urais Uganda kitaamuliwa na Bunge
Sep 14, 2017 10:14Rais Yoweri Museveni wa Uganda amejitosa kwenye mjadala kuhusu kikomo cha umri wa kugombea urais nchini humo na kusisitiza kuwa, kauli ya mwisho kuhusu kadhia hiyo itatolewa na Bunge la nchi hiyo.
-
Mwito wa kutumiwa Kiswahili kuimarisha utangamano Afrika Mashariki
Sep 09, 2017 03:19Naibu Waziri Mkuu wa Uganda ametoa wito wa kutumiwa lugha ya Kiswahili kuimarisha utangamano katika kanda ya Afrika Mashariki.