-
Mshauri wa Amiri Jeshi Mkuu wa Iran atoa onyo kwa Marekani na Uingereza
Jul 24, 2019 13:25Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya ulinzi ametoa onyo kwa Uingereza kuhusiana na nia yake ya kujiingiza kwenye eneo la Lango Bahari la Hormuz na kwa Marekani kuhusu nia yake ya kutaka kuanzisha vita vya kijeshi na akaeleza kwamba: Kauli iliyotolewa na Saudi Arabia na Imarati kuhusu kuhitimishwa vita vya Yemen inadhihirisha kushindwa kwao katika vita hivyo.
-
Iran: Tumesimamisha meli moja tu ya mafuta ya Uingereza kwa kuvunja sheria za kimataifa
Jul 19, 2019 22:45Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran IRGC limetangaza kuwa limesimamisha meli moja ya mafuta ya Uingereza baada ya kukiuka sheria za kimataifa za ubaharia katika Lango Bahari la Hormuz.
-
Tehran yaitaka Uingereza ijiepushe na mchezo hatari, iiachilie meli ya mafuta ya Iran
Jul 12, 2019 20:37Iran imeitaka Uingereza iachilie mara moja meli yake kubwa ya mafuta iliyokamatwa katika lango bahari la Jabal Tariq (Gibraltar) na imeitahadharisha London juu ya kuingia katika mchezo hatari usio na mwisho.
-
Kusimamishwa meli ya mafuta ya Iran na utegemezi wa Uingereza kwa Marekani
Jul 12, 2019 09:33Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kusimamishwa meli ya mafuta ya Iran katika lango bahari la Jabal Tariq (Gibraltar) ni kielelezo cha utegemezi wa Uingereza kwa Marekani.
-
Kamanda wa IRGC: Uingereza na Marekani zitajuta kwa kuizuilia meli ya mafuta ya Iran
Jul 11, 2019 21:56Naibu Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) ameonya kuwa, Uingereza na Marekani zitajuta kutokana na hatua ya London ya kusimamisha na kuzuilia meli ya mafuta ya Iran katika Lango Bahari la Jabal Tariq (Gibraltar).
-
Trump na balozi wa Uingereza washambuliana kwa maneno
Jul 08, 2019 03:16Rais Donald Trump amemshambulia vikali balozi wa Uingereza mjini Washington aliyemtaja kiongozi huyo wa Marekani kama mtu mtepetevu, asiye na tajriba na anayeendesha Ikulu ya White House kishaghalabaghala.
-
Waziri wa Ulinzi wa Iran: Hatutaruhusu uharamia wa Uingereza
Jul 08, 2019 02:15Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria hatua ya askari wa Jeshi la Wanamaji la Uingereza ya kuisimamisha meli ya mafuta ya Iran katika Lango Bahari la Jabal al Tariq (Gibraltar) na kueleza bayana kuwa, Tehran kamwe haitaruhusu uharamia huo wa London.
-
Kuisimamisha meli ya mafuta ya Iran, chokochoko za Uingereza katika uwanja wa Marekani
Jul 05, 2019 08:00Askari wa Jeshi la Wanamaji la Uingereza jana Alkhamisi waliisimamisha meli ya mafuta ya Iran katika Lango Bahari la Jabal al Tariq kwa madai kwamba ilikuwa inaelekea Syria.
-
Saudia iliiomba Uingereza iishambulie kijeshi Iran, baada ya Marekani kukwepa kufanya hivyo
Jun 22, 2019 08:34Mkuu wa Idara ya Ujasusi wa Saudi Arabia aliiomba serikali ya Uingereza ishambulie kambi na vituo vya kijeshi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, masaa machache baada ya Rais Donald Trump wa Marekani kutangaza kuwa amesitisha kile alichokitaja kama shambulizi la ulipizaji kisasi la Washington dhidi ya Tehran.
-
Mahakama: Uingereza imekiuka sheria kwa kuiuzia silaha Saudia
Jun 21, 2019 00:04Mahakama ya Rufaa nchini Uingereza imesema kuwa serikali ya London ilikiuka sheria kwa kuiuzia silaha Saudi Arabia na washirika wake katika vita vya Yemen.