-
Dunia yaendelea kukosoa azimio la Seneti ya Ufaransa kuhusu marufuku ya hijabu
Apr 10, 2021 23:06Watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini Ufaransa na maeneo mengine ya dunia wameanzisha kampeni iliyopewa jina la Hands Off My Hijab (@handsoffmyhijab) wakieleza hasira zao dhidi ya azimio la Baraza la Seneti la Ufaransa la kuzidisha vizuizi na marufuku dhidi ya vazi la staha la mwanamke wa Kiislamu, Hijabu. Watu wengi wamesema kuwa azimio hilo linapiga vita Uislamu.
-
Muslim Advocates yaitaka Facebook ikomeshe chuki dhidi ya Uislamu
Apr 09, 2021 22:05Taasisi ya Muslim Advocates imewasilisha mashtaka mahakamani dhidi ya Facebook, Mkurugenzi Mtendaji wake, Mark Zuckerberg na kiongozi nambari mbili wa kampuni hiyo, Sheryl Sandberg ikiitaka Facebook kutilia maanani harakati zinazoeneza chuki na uhasama dhidii ya Waislamu katika mtandao huo.
-
Jumuiya ya Wasomi wa Kiislamu yalaani ombi la Ufaransa la misikiti kubariki ndoa za mashoga
Mar 27, 2021 22:46Jumuiya ya Kimataifa ya Wanazuoni wa Kiislamu imelaani wito wa serikali ya Ufaransa iliyowataka maimamu wa misikiti nchini humo kubariki na kuhalalisha ndoa baina ya mashoga na watu wenye jinsia moja, ikisisitiza kuwa wito huo unaonyesha msimamo wa kindumakuwili dhidi ya Uislamu.
-
Kuendelea chuki za rais wa Ufaransa dhidi ya Uislamu
Nov 22, 2020 21:34Ikiwa ni kuendeleza chuki zake dhidi ya Uislamu na Waislamu, rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, sasa ametoa muhula maalumu kwa viongozi wa makundi ya Kiislamu ya nchi hiyo kuhakikisha wanajivika utamaduni wa Magharibi hata katika mambo ambayo ni haramu kwa mujibu wa mafundisho ya dini tukufu ya Kiislamu.
-
Erdogan: Dunia ipige vita uadui dhidi ya Uislamu sawa ilivyo katika suala la kupiga vita Uyahudi
Nov 02, 2020 23:15Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki ameitaka dunia ijifunze na kupata somo na ibra kutokana na uzembe wa jamii ya kimataifa iliyoacha kuzuia mauaji ya kimbari ya Waislamu wa Bosnia Herzegovina na kusisitiza kuwa, dunia inapaswa kupiga marufuku na kupambana na chuki na uhasama dhidi ya Uislamu kama ilivyopambana na chuki dhidi ya Uyahudi baada ya Holocaust (yanayodaiwa kuwa mauaji ya Mayahudi wakati wa Vita vya Pili vya Dunia).
-
Waziri Mkuu wa Canada apingana na Macron, asema Uislamu hauna mfungamano na ugaidi
Oct 30, 2020 05:24Waziri Mkuu wa Canada, Justin Trudeau amesema kuwa gaidi aliyetekeleza hujuma ya kigaidi katika mji wa Nice nchini Ufaransa hawakilishi dini ya Uislamu wala Waislamu, na kwamba watu wote wanapasa kukiri ukweli huo.
-
Radiamali ya kindumakuwili ya Ufaransa kufuatia malalamiko ya Waislamu duniani
Oct 28, 2020 04:11Waislamu duniani kote wamekasirishwa na kushadidi vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa hasa cha kuchapishwa tena katuni zinazomvunjia heshima Mtume Muhammad SAW. Hasira za Waislamu zimeongezeka maradufu baada ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kutetea vitendo hivyo vya chuki dhidi ya Uislamu kwa kisingizo cha uhuru wa maoni.
-
Pogba 'ajiuzulu' timu ya taifa ya Ufaransa kufuatia matamshi ya Macron dhidi ya Uislamu
Oct 26, 2020 08:21Mchezaji nyota wa soka, Paul Pogba ameripotiwa kujiuzulu katika timu ya taifa ya soka ya Ufaransa, kutokana na matamshi yaliyotolewa na Rais Emmanuel Macron wa nchi hiyo ya Ulaya dhidi ya Uislamu, wakati akitetea vitendo vya kutusiwa na kuvunjiwa heshima Mtume Muhammad (SAW).
-
Erdogan: Rais wa Ufaransa apimwe uwezo wake wa kiakili baada ya matamshi yake dhidi ya Waislamu
Oct 25, 2020 09:21Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki amesema kuwa Rais wa Ufaransa, Emanue Macron, anahitaji kupimwa uwezo wake wa kiakili baada ya matamshi ya kibaguzi aliyotoa karibuni kuhusu dini ya Uislamu.
-
Waislamu wa Ufaransa wamjia juu Macron kwa matamshi yake dhidi ya Uislamu
Oct 07, 2020 04:26Waislamu nchini Ufaransa wamekosoa vikali kauli ya Rais Emmanuel Macron wa nchi hiyo kuhusu Uislamu na kusisitiza kuwa, matamshi ya rais huyo ni ya kibaguzi.