-
Russia: Kuna ushahidi mpya unaoonyesha kuwa Ukraine inafadhili ugaidi katika nchi kadhaa za Afrika
Oct 09, 2025 13:24Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia Maria Zakharova amesema, kuna ushahidi mpya unaoonyesha kuwa Ukraine inayasaidia makundi ya wanamgambo na ya kigaidi katika eneo la Sahara-Sahel barani Afrika, ikiwa ni pamoja na kuyasambazia ndege zisizo na rubani,
-
Putin aonya: Kuipatia Ukraine makombora ya Tomahawk kutavuruga uhusiano wa Russia na Marekani
Oct 06, 2025 02:22Rais Vladimir Putin wa Russia amesema ikiwa Marekani itaipatia Ukraine makombora aina ya Tomahawk ili kufanyia mashambulio ya masafa marefu ndani ya Russia, hatua hiyo itapelekea kuvurugika husiano wa Moscow na Washington.
-
FIFA iliyoipiga marufuku Russia kwa sababu ya vita vya Ukraine yasema haiwezi kuchukua hatua dhidi ya Israel
Oct 03, 2025 10:34Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Gianni Infantino amesema, taasisi hiyo haiwezi kutatua ‘masuala ya kijiopolitiki’, licha ya kuendelea kuandamwa na mashinikizo kimataifa ya kuitaka isimamishe uanachama wa Israel kutokana na vita vya kinyama na mauaji ya kimbari unayoendelea kufanya utawala huo wa kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ghaza, ambayo hadi sasa yameshateketeza roho za watu zaidi ya 65,000, wengi wao wakiwa wanawake na watoto.
-
Trump azishambulia China na India kwa kuziita 'wafadhili wakuu' wa vita vya Ukraine
Sep 25, 2025 04:12Rais wa Marekani Donald Trump amezituhumu India na China kuwa "zinafadhili kifedha" vita vya Ukraine kupitia uagizaji wa nishati kutoka Russia. Trump ametoa shutuma hizo katika hotuba yake kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa unaoendelea mjini New York.
-
Kamanda Mkuu wa Ukraine akiri: Warussia wametushinda katika mstari wa mbele wa vita kwa zana na nguvukazi
Sep 09, 2025 10:27Kamanda Mkuu wa jeshi la Ukraine Aleksandr Syrsky amesema jeshi la Russia limelizidi nguvu jeshi lao katika mstari wa mbele wa vita kwa zana na nguvukazi
-
Putin: Wanajeshi wa NATO nchini Ukraine watakuwa 'shabaha halali' ya Russia
Sep 05, 2025 11:03Rais Vladimir Putin wa Russia amepinga mapendekezo ya 'dhamana ya usalama ya nchi za Magharibi kwa Ukraine' akionya kwamba, wanajeshi wowote wa kigeni watakaotumwa katika nchi hiyo jirani watakuwa "shabaha halali" ya jeshi la Russia.
-
Kansela wa Ujerumani azitaka nchi za Ulaya zijiandae kwa vita vya muda mrefu vya Ukraine
Aug 30, 2025 05:52Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz amesema nchi za Ulaya zinapaswa zijiweke tayari kwa vita vya muda mrefu nchini Ukraine kutokana na kile alichokiita kusitasita kwa Russia kushiriki katika mazungumzo.
-
Russia: Tumepiga Ukraine kwa makombora ya hypersonic
Aug 29, 2025 02:23Russia imetangaza habari ya kutekeleza mashambulizi ya masafa marefu dhidi ya shabaha za jeshi la Ukraine, kwa kutumia aina mbalimbali za silaha, yakiwemo makombora ya hypersonic aina ya Kinzhal.
-
Ubelgiji kupiga marufuku simu za mkononi maskulini kuanzia mwaka wa masomo wa 2025-2026
Aug 19, 2025 06:12Matumizi ya simu za mkononi na vifaa vingine vya kielektroniki yatapigwa marufuku nchini kote Ubelgiji katika skuli za msingi na sekondari kuanzia mwaka wa masomo wa 2025-2026, isipokuwa vitakapolazimu kutumika kwa sababu za kimasomo, kiafya, au za dharura. Hayo yameripotiwa na vyombo vya habari vya ndani ya nchi hiyo.
-
Trump na Putin wakutana Alaska bila ya kufikia mwafaka wa kusimamishwa vita vya Ukraine
Aug 16, 2025 05:07Duru ya kwanza ya mazungumzo kati ya Rais Vladimir Putin wa Russia na Rais wa Marekani Donald Trump iliyofanyika katika jimbo la Alaska nchini Marekani imemalizika pasi na kufikiwa mwafaka wa kusimamishwa vita vya Ukraine.