-
Rais wa Ukraine aliagiza jeshi liue 'makumi ya maelfu ya Warusi'
Jan 28, 2026 10:19Jeshi la Ukraine linapaswa lijikite katika kusababisha vifo vingi zaidi kwa Russia kadiri iwezekanavyo. Hayo yametamkwa na Rais wa Ukraine Vladimir Zelensky na kusisitiza kwamba, idadi ya vifo 50,000 vya Warusi kwa mwezi ni "kiwango bora" ambacho wanajeshi wa Ukraine wanapaswa wajitahidi kukifikia.
-
Iran yamjibu Zelensky; yamwambia dunia imechoka na 'vikaragosi vilivyochanganyikiwa'
Jan 24, 2026 03:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amemkosoa Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky kwa kuingilia masuala ya ndani ya Jamhuri ya Kiislamu, na kumwambia bayana kwamba dunia imechoka na "Wanaserere Waliochanganyikiwa."
-
Orban: Hungary haitaruhusu Ukraine kujiunga na EU miaka 100 ijayo
Jan 24, 2026 02:47Waziri Mkuu wa Hungary, Viktor Orban amesema kwamba Ukraine inajaribu kushawishi na kuathiri matokeo ya uchaguzi ujao wa bunge nchini Hungary, akisitiza kuwa nchi yake haitaruhusu Ukraine kujiunga na Umoja wa Ulaya katika miaka 100 ijayo.
-
Trump adai: Zelensky hana mpango wowote kwa ajili ya amani ya Ukraine
Dec 28, 2025 02:51Rais Donald Trump wa Marekani amesema kuwa Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine hana mpango wowote hadi yeye Trump aidhinishe.
-
Zelensky alemewa na mashinikizo ya Marekani ili kukubali mpango wa Trump wa kumaliza vita vya Ukraine
Dec 09, 2025 11:28Serikali ya Marekani imezidisha mashinikizo kwa Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ili kukubali kuachia sehemu kubwa ya ardhi ya nchi hiyo na makubaliano mengine yaliyoainishwa katika mpango wa amani wa mwenzake wa Marekani Donald Trump.
-
Changamoto za Umoja wa Ulaya katika kuchangisha fedha kwa ajili ya Ukraine
Dec 01, 2025 02:46Umoja wa Ulaya umekumbwa na changamoto nzito katika kuzishawishi nchi wanachama zikubali kuchangia fedha za kuendelea kuiunga mkono Ukraine kwenye vita vyao na Russia.
-
Nchi wanachama wa NATO kuilipa Marekani yuro milioni 400 za silaha itakazoipatia Ukraine
Nov 16, 2025 02:27Katibu Mkuu wa shirika la kijeshi la NATO Mark Rutte amesema, nchi kadhaa wanachama wa shirika hilo zitachangia kwa pamoja shehena ya silaha na zana za kijeshi yenye thamani ya yuro milioni 400 kwa ajili ya Ukraine, ambazo zitanunuliwa kutoka Marekani.
-
Ufaransa yatangaza kuwa tayari kutuma wanajeshi nchini Ukraine
Oct 26, 2025 10:19Pars Today- Mkuu wa Komandi Kuu ya Jeshi la Ufaransa ametangaza kwamba ikiwa Russia na Ukraine zitafikia makubaliano ya kusitisha mapigano, Paris itakuwa tayari kutuma wanajeshi nchini Ukraine kama sehemu ya kutoa dhamana za usalama kutoka kwa nchi za Magharibi.
-
Trump: Ukraine haiwezi kushinda vita dhidi ya Russia
Oct 21, 2025 11:26Rais wa Marekani, Donald Trump amesema haitakidi kwamba Ukraine inaweza kuibuka mshinda katika vita vyake na Russia.
-
Trump azitaka Russia na Ukraine zisimamishe vita mahali zilipo sasa hivi kwenye medani ya mapigano
Oct 20, 2025 09:40Rais wa Marekani Donald Trump ametoa wito kwa Russia na Ukraine kusimamisha vita katika mstari wa mapigano zilipo hivi sasa, pendekezo ambalo litaiwezesha Moscow kuhodhi sehemu kubwa ya maeneo ya ardhi ya Ukraine.